Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. MTOLEA aliuliza:- Bunge liliridhia nyumba za NHC zilizowekwa katika kundi A ziuwe, kundi B zikarabatiwe, kundi C zijengwe upya:- Je, kwa nini hadi leo baadhi ya nyumba zilizoagizwa kuuzwa hazijauzwa kwa wapangaji wake?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Nyumba limekuwa likiwapa notice wafanyabiashara eneo la Keko Furniture ambao wanafanya biashara chini ya majengo ya National Housing kwamba wahame wakatafute sehemu nyingine ya kufanyia biashara ili shirika izikarabati nyumba zile na iweze kuwapangisha wapangaji wengine. Wafanya biashara hawa ni zaidi ya 300 na shirika linataka liwafukuze ili lipangishe watu wasiozidi 50. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari sasa kulishauri Shirika la Nyumba wawe flexible badala ya kuwafukuza hawa watu 300, wavunje zile nyumba wajenge mabanda ambayo yatawa-accommodate hawa wafanyabiashara ili wawe wapangaji wao? Swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa na mchezo mchafu, watu ambao hawakai kwenye nyumba zile lakini ndiyo wanaonekana wapangaji wa nyumba za National Housing, kisha wao wanawapangisha watu wengine kwa gharama kubwa. Je, shirika litakuwa tayari sasa kufanya uhakiki wa kuhakikisha kwamba anayekaa kwenye nyumba ndiye ana mkataba na National Housing ili kuzifanya nyumba hizo zisiwe za gharama kubwa na zitumike na watu wenye mahitaji nazo? Ahsante.

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

Naibu Spika, ni kweli hayo anayoyasema ya wafanyabiashara wa Keko Furniture na hata juzi alikuja mmoja kuonesha vifaa vya hospitali hapa, nawajua, lakini kwa ufupi ningemshauri, mimi na yeye na baadhi yao tukipata fursa tukutane maana majibu yanaweza kuwa marefu hapa, tuone namna ya kutekeleza kwa pamoja ili kuwawezesha hawa vijana wafanyabiashara 500 waendelee kujiajiri katika eneo hilo. Sasa tutoke nje tuzungumze zaidi badala ya kukujibu hapa maana nitajibu majibu marefu sana, tutafute muafaka wa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, ni kweli shirika linafanya uhakiki. Hivi sasa ukiomba nyumba ya Shirika la Nyumba hupati, yule aliyepo anampa funguo mwenzake na hata wafanyabiashara wa maduka makubwa kama Samora na kadhalika wengine wanakula kodi za mtu wa tatu. Hilo nalijua na nimeshatoa maelekezo, kama unavyosema Mheshimiwa Mtolea, kwa National Housing wafanye uhakiki ili wachukue kodi kwa mpangaji na isitokee mtu mwingine kuchukua kilemba cha mpangaji. Kwa hiyo, hilo tunalifanyia kazi.