Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 19 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 164 2016-05-13

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. MTOLEA aliuliza:-
Bunge liliridhia nyumba za NHC zilizowekwa katika kundi A ziuwe, kundi B zikarabatiwe, kundi C zijengwe upya:-
Je, kwa nini hadi leo baadhi ya nyumba zilizoagizwa kuuzwa hazijauzwa kwa wapangaji wake?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Ally Mtolea, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba swali hili limekuwa likiulizwa sana kwenye Bunge hili, lakini nataka nimjulishe mdogo wangu, Mheshimiwa Abdallah Ally Mtolea kwamba hakujawahi kutolewa uamuzi rasmi wa Serikali wala Bodi ya Shirika au halijawahi kuwepo azimio rasmi la Bunge hili kufikishwa Serikalini kutaka Serikali kufikiria kuuza nyumba hizo ulizozitaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, utafiti uliofanywa mwaka 2010 ulionesha kuwa nyumba zinazomilikiwa na National Housing zina tija kubwa kwa Shirika na Taifa, hivyo nyumba hizo zilizotajwa hazitauzwa kwa kuwa ziko kwenye maeneo yenye thamani kubwa na ni mtaji wa kuliwezesha shirika kujenga nyumba nyingi zaidi zitakazowanufaisha wananchi wote na si wapangaji wachache. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la sasa la shirika ni kuendelea kuzifanyia matengenezo nyumba zake na kuvunja nyumba kama hizo ambazo mamlaka za manispaa na halmashauri mbalimbali zimezi-condemn nyumba hizo na zile zilizochakaa vilevile ili kujenga nyumba mpya za kisasa zitakazotoa fursa zaidi kwa Watanzania wengi kuuziwa wakiwemo wapangaji hao.