Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wafanyabiashara ili wafanye biashara zenye tija?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini napenda kumuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia soko lenye uhakika na tija nchini?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha akinamama kwenye mitandao ya wafanyabiashara duniani? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mwantumu kwa vile ambavyo anawasemea sana akinamama ili kuhakikisha nao wanajikomboa katika kufanyabiashara katika mazingira mazuri. Lengo la Serikali, kwanza ni kuhakikisha wafanyabiashara wote wakiwemo akinamama wanazalisha bidhaa zao katika ubora. Kwa hiyo, la kwanza tunalofanya kuhakikisha tunawapa mafunzo ili kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye tija.

Mheshimiwa Spika, pili, kupitia taasisi zetu tunawaunganisha kwenye masoko mbalimbali kupitia maonesho ambayo yanaandaliwa na TANTRADE. Pia kwenye kuhakikisha wanaingia kwenye mtandao wa wafanyabiashara duniani kwa kupitia chamber ya wafanyabiashara wanawake Tanzania Women Chamber of Commerce tumekuwa tukiandaa kwa kushirikiana na Serikali, ziara kwenye Maonyesho ya Kimataifa ikiwemo ile iliyofanyika mwaka 2018 kule China ili angalau kuwapa uelewa mpana kwa wafanyabiashara wetu akinamama katika masoko ya kimataifa.

Mheshimiwa Spika, pia zaidi sasa tumeanzisha biashara mtandao kupitia TANTRADE na Posta ili iwasaidie kufanya biashara kwenye mtandao na hivyo kujiongezea kipato. Nakushukuru sana.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wafanyabiashara ili wafanye biashara zenye tija?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali ililipa eneo la Viwanda na Uwekezaji pale Bunda Mjini kwa muda mrefu na wananchi wakahama kwenye eneo lile, lakini leo wameanza kurejea kwenye eneo lile. Ni nini mpango wa Serikali katika kulitumia eneo lile?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Robert Maboto, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli eneo lile ambalo lilo pale, lipo chini ya EPZA kwa maana ya maeneo ya uwekezaji huru kwa ajili ya mauzo nje. Serikali tunaendelea kutafuta fedha ili tuweze kuyaendeleza maeneo yote ambayo yapo chini ya EPZA likiwemo eneo hili la Bunda Mjini.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutalitekeleza au tutaanza kulifanyia kazi hivi karibuni katika eneo hilo la Bunda Mjini. Nakushukuru.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wafanyabiashara ili wafanye biashara zenye tija?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo nyongeza. Tuna Mifuko mingi sana ya uwezeshaji wanawake na vijana kiuchumi na mifuko hiyo imekuwa kwenye Wizara mbalimbali ndani ya Serikali: -

Kwa nini Serikali sasa isifikirie angalau kuwa na mifuko miwili ambayo itatosheleza mahitaji ya walengwa kwa maana ya wanawake na vijana? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Paresso kwa sababu anauliza swali la msingi sana kuona namna ambavyo tunaweza kupunguza wingi wa Mifuko hii ambayo inahudumia wananchi kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, tunalipokea wazo hili na Serikali ipo kwenye michakato kuona namna gani ya kuunganisha mifuko inayotoa huduma zinazofanana ili kuweza kuifanya iwe na tija kwa ajili ya kuwasaidia wananchi ikiwemo akina mama, vijana na walemavu. Kwa hiyo, tunachukua mawazo yake, nasi tunaendelea kuyafanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wafanyabiashara ili wafanye biashara zenye tija?

Supplementary Question 4

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuiuliza Wizara, kutokana na athari za UVIKO-19 nchi yetu pia imekumbwa na ongezeko la mfumuko wa bei: -

Je, Wizara imefanya tathmini gani kuona athari ambazo wafanyabiashara wamepata; na wana mkakati gani kuhakikisha hali ya mfumuko wa bei nchini unakwenda kurekebishwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bahati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli sote ni mashahidi kwamba kumekuwa na athari kubwa kutokana na janga hili la ugonjwa wa UVIKO-19, katika bidhaa mbalimbali kwa maana ya kupanda bei. Serikali inafanya jitihada za makusudi kuona namna gani tunasaidia viwanda na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali ndani ya nchi pamoja na kuweka vivutio na kupunguza gharama za wale ambao wanaingiza bidhaa mbalimbali zinazotumika kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, nadhani mtaona kwa makusudi Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuangalia hili, aliweza kuangalia pia eneo la mafuta ambayo ni sehemu nyeti sana inayoongeza gharama za bidhaa kwenye usafirishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, pamoja na mambo mengine tunaangalia kwa namna gani tutasaidia wazalishaji ili waweze kuzalisha kwa bei nafuu, na pia mnyororo mzima wa usafirishaji wa bidhaa za ndani na zile zinazotoka nje ya nchi. Nakushukuru sana. (Makofi)