Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Industries and Trade Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 153 2022-02-17

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia akinamama wafanyabiashara ili wafanye biashara zenye tija?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha wafanyabiashara wadogo wakiwemo akinamama kufanya shughuli zao katika maeneo rasmi na kuchukua vitambulisho vya wajasiriamali na kurasimisha biashara zao. Mikakati ya Serikali ni kuendelea kuwasaidia akinamama wafanyabiashara kupitia mikopo inayotolewa na Mifuko ya Uwezeshaji ukiwemo Mfuko wa Taifa wa Kuendeleza Wafanyabiashara Wananchi (NEDF) chini ya Shirika letu la Kuendeleza Viwanda Vidogo (SIDO) na Mfuko wa Dhamana ya Mikopo kwa Wajasiriamali (SME Credit Guarantee Scheme) unaoratibiwa na pia SIDO kwa kushirikiana na Benki ya CRDB.

Mheshimiwa Spika, pia tunaendelea kuboresha na kujenga miundombinu ikiwemo majengo ili wapate sehemu tulivu za kukuza biashara zao. Kuanzia Julai, 2015 hadi Machi, 2021, Serikali kupitia Mfuko wa Dhamana ya Mikopo kwa Wajasiriamali pekee imekwishawapatia akinamama wafanyabiashara mikopo yenye thamani ya Shilingi milioni 310. Aidha, Wizara inakamilisha mapitio ya Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo ya mwaka 2003 ili iweze kuendana na mabadiliko ya kijamii na kiuchumi ya sasa. Nakushukuru.