Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule za msingi kongwe ambazo zimechakaa na majengo yake ni mafupi ulikinganisha na yanayojengwa kwa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Wilaya hii ya Newala ni kati ya wilaya kongwe hapa nchini na shule zake mfano Shule ya Makukwe II, Nakaako na Babati ni shule ambazo zina hali mbaya na mapaa yake yake yanavuja hivi sasa. Kipindi hiki cha masika, vijana wetu wanasoma katika mazingira magumu sana. Swali la kwanza, Serikali itakuwa tayari kuzifikiria shule hizi katika mwaka ujao wa fedha kuipangia bajeti ya kutosha ili kufanya ukarabati?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; linakwenda ndani ya jimbo langu. Katika Kata ya Mikangaula, Wilaya ya Nanyumbu kuna shule ya Mikangaula ambayo ina wanafunzi 1,500 na kuna darasa lina wanafunzi 300. Kwa kutambua adha hii wananchi wa Kata hii wameamua kutumia nguvu zao ili kujenga madarasa katika vijiji vingine. Je, Serikali ipo tayari kushirikiana na wananchi wa Kata hii kuipatia fedha ili vijiji hivi ambavyo vimetoa nguvu zao waweze kupata fedha na kuwanusuru wananchi wao? (Makofi) Je, ni lini Serikali itakabidhi majengo yaliyokuwa ya Hospitali ya Muhimbili kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ili kupunguza uhaba wa majengo katika Hospitali hiyo.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli nimweleze tu kwamba Serikali ipo tayari kuingiza katika mpango Halmashauri ya Newala na kuhakikisha hizo shule kongwe zote zinafanyiwa ukarabati. Hapa nimweleze tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mpaka sasa hivi tathmini ya awali tumeshapata tathmini ya Shule 750 za Msingi Kongwe ambazo zimejengwa kabla ya mwaka 1950, yaani kabla ya uhuru wa nchi yetu ambazo tunatakiwa kuzifanyia tathmini.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wetu ni ndani ya miaka mitano shule zote kongwe nchini tutazikarabati kwa kujenga madarasa mapya, ndiyo maana katika mwaka wa fedha 2022/2023 tuna ujenzi wa madarasa kwenye Shule za Msingi 12,000 nchi nzima kwa ajili ya kwenda kufanya hayo maboresho. Kwa hiyo, tuko tayari kwa hilo ikiwemo na katika eneo la jimbo la Mheshimiwa katika Kata ya Mikangaula ambayo umeianisha kwamba tutaingiza katika mpango na tutawapatia fedha ili kumalizia hayo majengo. Ahsante sana.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule za msingi kongwe ambazo zimechakaa na majengo yake ni mafupi ulikinganisha na yanayojengwa kwa sasa?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa lengo ni kuboresha elimu yetu nchini. Ni kwa nini sasa Serikali isipandishe hadhi Shule ya Sekondari Sepuka ambayo ipo Jimbo la Singida Magharibi ambayo kwa sasa ndiyo shule kongwe kuliko shule zote katika Tarafa ya Sepuka ambayo imebeba nusu ya Kata za Jimbo la Singida Magharibi? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba ombi la Mheshimiwa Mbunge ni Shule ya Sepuka sijajua ni sekondari ama msingi, lakini naamini ni Sekondari kwenda Kidato cha Tano na cha Sita ambao wanataka tupandishe hadhi na kuwa kidato cha tano na cha sita kwa sababu inapokea wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali. Moja ya mpango wa Serikali ni kufanya upanuzi wa shule za sekondari za Kata 100 katika mwaka 2022 ili tuongeze wigo wa kuongeza wanafunzi wa kwenda kujiunga na kidato cha tano na cha sita.

Mheshimiwa Spika, naamini kama lipo katika mpango, basi maana yake tutalifanyia kazi katika mwaka huu fedha 2022/2023, lakini kama halipo maana yake tutalifanyia kazi katika mwaka wa fedha unaokuja 2023/2024. Kwa hiyo, nitayapitia ili niweze kujiridhisha nione kama halipo katika mwaka huu, kama litakuwepo mwakani maana yake tutaliingiza, kwa hiyo ni hilo tu. Ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule za msingi kongwe ambazo zimechakaa na majengo yake ni mafupi ulikinganisha na yanayojengwa kwa sasa?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, hali ilivyo kwenye Wilaya ya Newala ni sawasawa na Kibaha Vijijini kwenye shule za Dutumi, Madege na Magindu. Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati sahihi na kule kulifanyia ukarabati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumjibu Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika jibu la msingi kwamba mwakani tuna madarasa zaidi 12,000 kwa ajili ya ukarabati wa shule za msingi nchini. Kwa hiyo, naamini kwa sababu moja ya utaratibu wetu ni kuhakikisha kwamba tunayafikia majimbo nchini, likiwemo Jimbo la Kibaha Vijijini. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge aondoe wasiwasi kwa sababu tutaweka katika mpango na wananchi wake watapata hiyo faida ya yeye kuwepo ndani Bunge. Ahsanteni sana kwa kunisikiliza. Ahsante sana.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule za msingi kongwe ambazo zimechakaa na majengo yake ni mafupi ulikinganisha na yanayojengwa kwa sasa?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa shule ya Sekondari ya Sumve ni moja ya shule kongwe ambayo ina historia kubwa sana kwenye nchi yetu ambapo mama Maria Nyerere alipata elimu yake pale na ni shule ambayo imechakaa sana. Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuipa kipaumbele shule hii ya Sumve Sekondari katika kuanza ukarabati wa shule kongwe katika bajeti inayokuja?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumjibu kwa kifupi sana Mheshimiwa Kasalali kwa swali lake; ni kwamba shule aliyoitaja Sumve ambayo ina historia kubwa amesema tuipe kipaumbele basi na mimi nilipokee ombi lake tutazingatia, tutampa kipaumbele na kama tutakavyowapa Wabunge wote katika Bunge hili. Ahsante sana. (Makofi)