Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 151 2022-02-17

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa shule za msingi kongwe ambazo zimechakaa na majengo yake ni mafupi ulikinganisha na yanayojengwa kwa sasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa shule kongwe za msingi zilizo katika hali ya uchakavu. Kazi ya kuzikarabati shule hizi ilishaanza kupitia miradi mbalimbali ya elimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya elimu kwa kujenga na kukarabati miundombinu mbalimbali ya shule za msingi nchini. Katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali kupitia Programu ya EP4R (Lipa Kulingana na Matokeo) imeendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa ya shule za msingi 1,970, matundu ya vyoo 5,303, nyumba za walimu wa msingi 17. Ujenzi huu ni kwa ajili ya kuboresha mazingira ya miundombinu ya shule za msingi zikiwemo shule kongwe ambazo zina miundombinu chakavu. Vilevile kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 (TCRP), Serikali imejenga vyumba 3,000 vya madarasa katika vituo shikizi 970.

Mheshimiwa Spika Serikali kupitia Mradi wa BOOST utakaotekelezwa katika shule za msingi inatarajiwa kujenga madarasa 12,000 katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 na itaendelea kutumia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri kujenga na kukarabati shule za msingi kongwe nchini.