Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Malinyi?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanafunzi ambao wanamaliza kKidato cha nne Wilaya ya Malinyi ambao hawaendelei na masomo ya Kidato cha Tano wako zaidi ya 600 kila mwaka; na wengi wao kimbilio lao lilikuwa ni kilimo; na sasa kutokana na mgogoro kati ya Wizara ya Maliasili (TAWA na wananchi wa Malinyi) kuna uwezekano mkubwa tukapoteza maeneo ya kulima. Wanafunzi hao wanahitaji ujuzi wa ziada kwa ajili ya kujikwamua nje ya kilimo:-

Je, Serikali haioni haja ya kuiingiza Malinyi katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, anayoyazungumza Mheshimiwa Mbunge ni kweli, uhitaji wa vyuo hivi ni mkubwa sana sio tu kwa Malinyi. Kama nilivyozungumza kwenye jibu langu la msingi kwamba tunamalizi ujenzi wa vyuo hivi 25 katika wilaya 25 pamoja na mikoa minne nimuondowe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge katika bajeti ijayo iwapo Serikali tutapata fedha kipaumbele cha kwanza itakuwa ni eneo hili la Malinyi na maeneo mengine ambayo yenye uhitaji mkubwa ukilinganisha na maeneo mengine tayari yanavyuo karibu.