Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 148 2022-02-16

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Malinyi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi n a Teknolojia naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Jimbo la Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na mpango wa ujenzi wa vyuo vya mafunzo na ufundi stadi katika Mikoa na Wilaya kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sasa Serikali inakamilisha ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya 25 na Mikoa minne nchini kwa lengo la kuwapatia vijana ujuzi katika fani mbalimbali utakaowawezesha kuajiriwa au kujiajiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi ambacho Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya ya Malinyi na maeneo mengine, wananchi wa Malinyi wanashauriwa kutumia Vyuo vya VETA vilivyopo katika Mkoa wa Morogoro ambavyo ni Mikumi, Dakawa, Kihonda, Ulanga pamoja na vyuo vingine vya VETA vilivyopo nchini kwa ajili ya kupata elimu na mafunzo ya ufundi. Nakushukuru sana. (Makofi)