Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni kwa nini Mfuko wa Pembejeo ambao ulianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima wadogo waliopo Vijijini haupokei Hati za Kimila ambazo ndizo zilizopo Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa hii nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule kwetu Mbozi wakulima wetu wamefungiwa, hawawezi kwenda kukopa kwenye Mfuko wa Pembejeo na sababu ni hao wakulima 28 ambao hawajarejesha mikopo kwenye huo Mfuko wa Pembejeo.

Je, Serikali haioni kwamba haitendi haki kuwazuia wakulima wote wa Wilaya ya Mbozi, kutokupewa nafasi ya kukopa kwenye huu mfuko kwa ajili ya hao wakulima 28? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kilimo ndiyo uti wa mgongo kwenye Taifa letu. Kwa nini basi ni ngumu kwa mkulima hasa aliyepo vijijini kukopesheka ndani ya nchi hii? Nini mkakati wa Serikali kumwekea mazingira mazuri huyu mkulima aweze kukopa kwa urahisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba tu kwamba baada ya Bunge aidha ni leo au kesho tuweze kukutana tujadili suala la wakulima wake wa Mbozi kama special case na tuweze kutafuta solution ya kudumu kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ambalo nataka niseme ni kweli mfumo wa fedha katika nchi yetu na mifumo ya kukopesha katika nchi yetu sio rafiki kwenye sekta ya Kilimo. Kwa hiyo, kama Wizara ya Kilimo hatua tuliyochukua sasa hivi tumeanza maongezi na wenzetu Wizara ya Fedha na vile vile kuwahusisha Banki Kuu ya Tanzania, ili tuwe na sera ya fedha ya kukopesha wakulima. Kwa sababu sera zetu za fedha na sheria zetu za mikopo zinazo guide financing kwenye uchumi na kutoa mikopo nyingi zimekaa kuitazama kama grocery ndio hivyo hivyo na sekta ya kilimo inavyotazamwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tumekubaliana na wenzetu Wizara ya Fedha ili kuja na financing na policy ya agriculture financing na SME ili iwe rafiki kuwakopesha wakulima wakati huo huo tayari tunayo instrument ya TADB, kwa sababu sasa hivi tunatumia kukopesha kutokana na case by case. Kwa hiyo, tunataka tuwe na legal frame work ili iweze kusimamia suala la ukopeshaji wa sekta ya kilimo na vile vile ukopeshaji wa value chain ya kilimo na tuwe na legal procedure ambayo inaweza kuzifanya taasisi za fedha ziweze kuifata na zisimtazame mkulima kama muuza duka wa kawaida. (Makofi)