Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 131 2022-02-15

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: -

Je, ni kwa nini Mfuko wa Pembejeo ambao ulianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima wadogo waliopo Vijijini haupokei Hati za Kimila ambazo ndizo zilizopo Vijijini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Mwenisongole Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka, 2005 hadi 2010, Mfuko wa Pembejeo uliwahi kupokea hati za kimila kama dhamana kwa majaribio, ambapo Wilaya ya Mbozi ndiyo iliyokuwa pilot study kwa ajili ya kupewa hati hizo. Baada ya kutoa mikopo hiyo, Mfuko wa Pembejeo ulikabiliwa na changamoto ya mikopo kutofanyiwa marejesho. Aidha, Mfuko wa Pembejeo ulipojaribu kuuza mashamba hayo ilishindikana kwa ajili ya kufidia mikopo, iliyotolewa; haukufanikiwa kutokana na mashamba hayo kuwa ya jamii au ya ukoo unaoishi pamoja na siyo la yule mwenye hati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, katika Wilaya ya Mbozi, Mfuko ulitoa mikopo yenye thamani ya shilingi 480,422,335 kwa wakulima 28. Kati ya fedha hizo shilingi 135,947,935 zilirejeshwa na shilingi 344,563,400 bado hazijarejeshwa mpaka sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto zilizojitokeza, Bodi ya Wadhamini mwaka, 2016 ilisitisha utoaji wa mikopo kwa kutumia hati hizi kama dhamana, mpaka hapo zitakapofanyiwa marekebisho kwenye Sheria ya Ardhi ya Vijiji (The Village Land Act) ili kuondoa changamoto hizo. (Makofi)