Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Uwanja wa Ndege wa Ipole pamoja na nyumba ya kupumzikia wageni wanaokuja kwa ajili ya utalii wa picha na kuangalia Wanyama kwenye WMA ya JUHIWAI, Mbuga za Ipembampazi na Isuvangala utajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza, napongeza majibu mazuri ya Serikali. Labda kabla sijauliza maswali ya nyongeza, nina maelezo ya ziada kwamba eneo la Uwanja wa Ndege wa Ipole liko chini ya Ofisi ya TAWA Kituo cha Ipole cha Pori la Akiba la Ugalla. Nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa kutoka Tabora mpaka Ipole ni kilomita 100; na kutoka Koga mpaka Ipole WMA ni kilomita 90: Je, Serikali haioni kwamba kujenga uwanja huo wa ndege pale Ipole kutakuwa na faida zaidi katika kuvutia watalii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: kwa kuwa huyu mwekezaji ameshajenga uwanja mdogo pale Koga na inaonekana kabisa Serikali haina nia ya kuendeleza ujenzi wa Uwanja wa Ndege pale Ipole: Je, Serikali iko tayari kuyarudisha mashamba na ardhi ya wananchi wa Ipole waliyoitoa mwaka 1996 kwa nia njema kwa Serikali kwa ajili ya kujenga Uwanja wa Ndege, kuwarudishia ili waendelee na shughuli zao za kiuchumi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza sana Mheshimiwa Kakunda kwa kuwa mhifadhi na pia ameendelea kuhamasisha utalii, ikiwemo maeneo haya yaliyopo katika Wilaya ya Sikonge hasa katika Pori la Akiba la Ugalla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kutoka Tabora mpaka Ipole ni kilomita 100 ambazo huwa zinasaidia watalii wanaofika Tabora kuelekea katika eneo hili la WMA. Sambamba na hilo, Mheshimiwa Kakunda ameomba Serikali iweze kujenga kiwanja katika eneo la Ipole ili kurahisisha watalii waweze kupita njia ambayo ameisema ya kilomita 90.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshauri tu kwamba maeneo yenye uhitaji ni mengi; na kwa kuwa kiwanja cha Tabora kinatosheleza maeneo haya kwa hizo kilomita alizozisema, basi naomba wananchi au wawekezaji waliopo katika maeneo hayo, waendelee kuvumilia wakati tunaangalia namna ya kuweza kuboresha, kiwanja kidogo kilichopo katika Kituo cha Ipole ili kuwawezesha wale watalii wanaotaka kuingia kwenye hiyo WMA ama kwenda kwenye Pori la Akiba la Ugalla waweze kufika kwa urahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tu kwamba Pori la Akiba la Ugalla limeshapata mwekezaji na tayari huyo mwekezaji yupo tayari kuendelea kuboresha kiwanja hicho. Hata Serikali tutajipanga katika maeneo hayo kuhakikisha kwamba tunaboresha viwanja hivyo ili kurahisisha watalii waweze kufika katika maeneo hayo. Ahsante (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Uwanja wa Ndege wa Ipole pamoja na nyumba ya kupumzikia wageni wanaokuja kwa ajili ya utalii wa picha na kuangalia Wanyama kwenye WMA ya JUHIWAI, Mbuga za Ipembampazi na Isuvangala utajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Mahitaji ya uwanja katika Wilaya ya Sikonge ni sawa kabisa na mahitaji, ambayo yapo katika Jimbo letu la Biharamulo ikizingatiwa kwamba Hifadhi ya Burigi, Chato ipo Biharamulo na mageti yote yapo Biharamulo; hata hivyo, tumekuwa na uwanja wetu wa muda mrefu pale eneo la Katoke ambao ungesaidia zaidi kukuza utalii hasa kwa wageni ambao watahitaji kutembelea Hifadhi ya Biharamulo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu: Ni lini mpango wa Serikali kusogeza huduma pale katika eneo la Katoke kwa kukarabati ule uwanja ili uweze kutumika na watalii wanaotembelea hifadhi yetu? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, namshukuru sana Mheshimiwa Engineer Ezra kwa kuwa ni mdau mkubwa wa kuhamasisha utalii katika maeneo ya Burigi Chato; na hili ni eneo mojawapo ambalo tumeendelea kulihamasisha; na kwa bahati nzuri sasa hivi tumeshaanza kupata watalii wengi katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakumbuka kwamba tuna kiwanja kizuri sana ambacho kimejengwa na Serikali maeneo ya Chato. Uwanja huu ni mkubwa ambao ulikuwa na lengo la kuhakikisha wale watalii wote ambao wanataka kuingia lango la Chato na Biharamulo waweze kufika kwa urahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliweka mkakati kwamba pamoja na watalii wengi wanaopita maeneo hayo, wengi wao wakiwa wanunuzi wa madini, basi wanapopita kwenda kununua madini na uwanja wa ndege wa Taifa uko pale, basi ni rahisi kupita maeneo yale na pia kuona vivutio vilivyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, namwomba Mheshimiwa Eng. Ezra awe na subira kidogo wakati tunaangalia mafungu mbalimbali ya kuweza kuboresha eneo hili la Biharamulo – Katoke, tuendelee kutumia huu uwanja wa Taifa uliopo ambao ni mzuri zaidi kwa ajili ya kuwezesha watalii waweze kuingia katika malango haya yote mawili. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Uwanja wa Ndege wa Ipole pamoja na nyumba ya kupumzikia wageni wanaokuja kwa ajili ya utalii wa picha na kuangalia Wanyama kwenye WMA ya JUHIWAI, Mbuga za Ipembampazi na Isuvangala utajengwa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mbuga ya Serengeti ni maarufu sana duniani na watalii wengi sana huvutiwa kuja kutembelea mbuga ile, lakini kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwepo ukosefu wa uwanja wa ndege: -

Mheshimwia Mwenyekiti, kwa kuwa tangu Bunge la Kumi chini ya Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Wasira, tumekuwa tukifuatilia Serikalini kuhakikisha kwamba ile mbuga ndani ya Serengeti inajengwa uwanja wa kimataifa ili watalii wanaotoka nchi nyingine waje moja kwa moja watue kwenye huo uwanja wa kimataifa wa Serengeti kuliko ilivyo sasa hivi ambapo wanapita Kenya kwa njia za barabara: Ili kuongeza mapato ya nchi, kwa nini Serikali haioni umuhimu sasa wa kujenga uwanja wa Serengeti kuwa uwanja wa Kimataifa? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge kutoka Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Esther kwa kuendelea kuwa mdau katika Hifadhi ya Serengeti. Tunamshukuru sana kwa sababu ameendelea kutoa mchango mzuri katika Taifa letu ikiwemo Mbuga hii ya Serengeti ambayo imekuwa ikiongoza Kimataifa na duniani kote kama ni Mbuga bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe wasiwasi Mbunge kuhusu suala la ujenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha ndege ambacho Serikali inafikiria kujenga. Suala hili tumepanga kuweka uwanja wa ndege wa Kimataifa kwenye Wilaya ya Mugumu; na tayari Serikali tumeshapeleka maombi ya kuandaa eneo kubwa la uwekezaji, likiwemo eneo la uwanja wa ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tunalishanya kwa sababu wenzetu majirani tayari wameshaanza mchakato wa ujenzi wa uwanja wa kimataifa na lengo ni kuiua Mbuga ya Serengeti kwa kuleta watalii upande wao, lakini pia iwe rahisi kuingiza Tanzania. Nasi tumeona ni bora sasa tukaingia kwenye ushindani ikiwemo kujenga uwanja huu wa kimataifa ili ndege zinapokuja ziende moja kwa moja kwenye Hifadhi yetu ya Taifa ya Serengeti na moja kwa moja iwe rahisi kuingia kwenye Hifadhi ya Serengeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tunafanya hivyo ili kupunguza kelele na miungurumo mbalimbali inayofanyika kwenye uwanja mdogo ule wa Seronera ambao umekuwa ni kero kwa wanyama na hata kiuhifadhi. Hivyo, tunataka kuuhamishia maeneo ya Mugumu ili iwe rahisi kuleta wasafiri/watalii mbalimbali wanaotoka nje ya nchi waje kwa ajili ya kutuletea mapato nchini. Ahsante. (Makofi)