Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 129 2022-02-15

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Uwanja wa Ndege wa Ipole pamoja na nyumba ya kupumzikia wageni wanaokuja kwa ajili ya utalii wa picha na kuangalia Wanyama kwenye WMA ya JUHIWAI, Mbuga za Ipembampazi na Isuvangala utajengwa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa wageni wanaokwenda Ipole WMA kufanya shughuli za utalii wanatumia uwanja wa ndege wa Tabora, pamoja na kiwanja kidogo cha Koga kilichopo katika eneo la WMA. Hata hivyo, Serikali itaendelea kuhamasisha wawekezaji wanaowekeza katika maeneo hayo kujenga uwanja wa ndege pamoja na nyumba ya kupumzikia wageni ili kuhakikisha wageni wanaokwenda kwenye WMA ya Ipole, Mbuga za Ipembampazi na Isuvangala kwa ajili ya utalii wanaofika katika eneo husika bila tatizo.