Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuanzisha Wilaya mpya ya Kisesa Mkoani Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pia naomba niipongeze Serikali kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuanzisha mamlaka mapya ya utawala ni kusogeza huduma kwa wananchi, na suala hili limeletwa leo lina mwaka mzima uchambuzi unaendelea. Je, ni lini sasa wananchi hawa watapata jibu sahihi kwamba wilaya yao ianze mara moja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzisha mamlaka mpya ni kweli kunasogeza huduma karibu zaidi na wananchi, lakini pia kuna gharama mbalimbali ambazo zinaendana na kuanzisha makao mapya ya halmashauri. Na ndiyo maana halmashauri nyingi ambazo zimeanzishwa na maeneo mengine ya utawala bado Serikali inawekeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, ujenzi wa majengo ya utawala halmashauri, ujenzi wa ofisi mbalimbali za maeneo hayo ili kuwezesha wananchi kupata huduma bora kupitia ofisi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunakwenda kwa hatua, tuko hatua hii, tunakamilisha maeneo hayo na baadaye tutakwenda kwenye halmashauri nyingine na sisi tutashauri mamlaka kadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuona uwezekano wa kuanzisha mamlaka hizi. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuanzisha Wilaya mpya ya Kisesa Mkoani Mwanza?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mbulu Vijijini tumeshapata halmashauri na majengo yameshakamilika, na kwa kuwa Mbulu ina halmashauri mbili; je, lini mnatupatia mamlaka ya kuwa na wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu ina Halmashauri ya Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Vijijini. Na halmashauri hizi zote zinaendelea kuwekewa miundombinu ya ujenzi ikiwepo Halmashauri ya Mbulu Vijijini ambako jengo la kisasa kabisa la utawala limejengwa, limekamilika na hatua hiyo itawezesha halmashauri hii kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa halmashauri zile mbili na kwa ukubwa wa jiografia ile, tunafikiri bado tunastahili kuboresha kwanza halmashauri zilizopo na baadae kama kutakuwa na sababu ya kuanzisha halmashauri nyingine basi tathmini itafanyika na wananchi watapewa taarifa hiyo. Ahsante.