Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 123 2022-02-15

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuanzisha Wilaya mpya ya Kisesa Mkoani Mwanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mwanza uliwasilisha mapendekezo ya kuanzisha Wilaya ya Bujora (Kisesa) kupitia barua ya tarehe 15 Machi, 2021 na tarehe 10 Mei, 2021. Ofisi ya Rais – TAMISEMI inaendelea na uchambuzi wa mapendekezo ya kuanzisha wilaya hiyo na maeneo mengine ya utawala yaliyowasilishwa. Uchambuzi wa taarifa hizo utakapokamilika timu ya wataalam itatumwa kufanya uhakiki na baadae kuishauri mamlaka ipasavyo juu ya suala hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge na wananchi wawe na subira katika kipindi ambacho Serikali inaendelea na uchambuzi na tathmini ya taarifa zilizowasilishwa.