Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawalipa posho ya masaa ya ziada Watumishi wa afya waliofanya kazi kubwa sana katika kuokoa maisha ya Watanzania wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19?

Supplementary Question 1

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali; na niwapongeze kwa kutenga hizo fedha na kuzipeleka kwa ajili ya kufanya malipo; lakini nina maswali mawili (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna watumishi ambao wamestaafu lakini walihusika kwenye zoezi hili, wengine wamepewa nafasi za uteuzi na walihusika kwenye zoezi hili: Je, Serikali mmejipangaje kuhakikisha hizi fedha zinafika kwa walengwa? (Makofi)

(b) Kwa kuwa ulipaji wa malipo ya Watumishi wa Afya ni endelevu, Serikali mmejipangaje kuwa mnawalipa kwa wakati? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nipokee pongezi zake nyingi kwa Serikali ambapo baada ya watumishi wale kufanya kazi hiyo, imehakikisha imepeleka shilingi bilioni tatu kwa ajili ya watumishi kupata haki zao. Pili, watumishi waliostaafu au watumishi waliopata teuzi mbalimbali ambao kwa wakati huu hawapo kwenye Halmashauri, bado taarifa zao zote za kiutumishi na haki zao zipo katika Halmashauri husika na baada ya kuchakata malipo hayo, watapata haki zao kwa sababu taarifa zote zipo kwenye Halmashauri. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taarifa zao zote zipo na malipo watayapata pale walipo kwa kadri wanavyostahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na utaratibu wa malipo kwa watumishi wa huduma za afya, ni zoezi endelevu na Serikali imeendelea kuboresha utaratibu wa kuhakikisha watumishi wanaofanya kazi masaa ya zianda wanalipwa kwa wakati. Kwa kweli hali kwa sasa inaendelea kuimarika na mpango huu ni endelevu, tutahakikisha kwamba tunatafuta fedha kwa wakati na kuhakikisha kwamba watumishi wale wanapata haki zao kwa wakati.