Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 122 2022-02-15

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawalipa posho ya masaa ya ziada Watumishi wa afya waliofanya kazi kubwa sana katika kuokoa maisha ya Watanzania wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitoa maelekezo kwa Mamlaka za Mikoa na Halmashauri kuandaa madai yote ya posho za masaa ya ziada wanazodai Watumishi wa Afya waliofanya kazi katika mapambano ya kukabiliana na janga la ugonjwa wa UVIKO-19. Serikali ilipokea na kuhakiki madai yaliyowasilishwa ambapo kiasi cha shilingi bilioni 3.44 ndicho kinachostahili kulipwa ikiwa ni stahili kwa watumishi na wazabuni. Kati ya madai hayo, kiasi cha shilingi bilioni tatu sawa na 87% tayari zimepelekwa kwa ajili ya kulipa madeni hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wowote taratibu za kifedha zitakapokamilika, madeni na stahili za watumishi na wazabuni zilizosalia zitalipwa. Aidha, nazielekeza Mamlaka za Mikoa na Halmashauri waliopelekewa fedha za madeni hayo wazisimamie na kuhakikisha kila mtumishi anapata stahiki yake. Ahsante.