Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa utoaji wa mbegu bora za alizeti ili kuongeza uzalishaji wenye tija kwa Wakulima katika Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri kutokana na suala la zao muhimu la alizeti katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo tani ambazo zimetajwa hapa tani 48 zilizosambazwa katika Mkoa wa Shinyanga na tani hizi za mbegu hazijaainishwa katika Wilaya ya Kishapu ni kiasi gani cha tani za mbegu ambazo zimesambazwa katika Wilaya ya Kishapu peke yake. Pengine katika maswali yangu ya nyongeza ni kwamba ASA ambaye ni Wakala aliyekuwa anashughulikia usambazaji wa mbegu katika Mkoa wa Shinyanga Wilaya ya Kishapu peke yake ni Wilaya ambayo ilibidi wakulima wapate huduma kutoka Kishapu kwenda Manispaa ya Mjini Shinyanga Makao Makuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; je, Serikali haioni haja ya kusogeza huduma hii ili ASA aweze kusambaza ama kutoa huduma katika Wilaya per se? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; lipo eneo katika Wilaya yetu ya Kishapu ambalo linamilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambayo ni zaidi ya ekari mia tatu. Je, Serikali ipo tayari kuja kuliona eneo hilo na ikiwezekana kuanzisha kilimo maalum cha zao la pamba kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu hizi za kisasa ili tuongeze tija na upatikanaji wa karibu zaidi kwa wananchi wa Kishapu kwa ajili la suala zima la mbegu za alizeti?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Butondo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwepo wa eneo la ekari 300 Serikali tupo tayari kushirikiana na Halmashauri husika ili tuweze kuona ni namna gani hilo eneo linaweza kutumika na kwa maslahi ya wananchi wa Kishapu, hivyo, milango ya Wizara ya Kilimo iko wazi karibu wewe na Mkurugenzi wako tuweze kujadiliana ni namna gani tunaweza kulitumia hilo eneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kusogeza huduma za ASA katika Halmashauri ya Kishapu. Ninataka tu nimuombe Mheshimiwa Mbunge na niwaombe Wabunge wote, siyo rahisi kuweka ofisi ya ASA katika kila Wilaya kwa wakati mmoja, gharama za uendeshaji zitakuwa kubwa na hazina economic value. Kama Halmashauri husika ina mahitaji specific ya mbegu, tupo tayari watuletee mahitaji yao, tuya- aggregate pamoja na tuwapelee katika ngazi ya Halmashauri ama Mkoa halafu wao wenyewe waweze kusambaza katika maeneo yao na wakulima wao kama tulivyofanya katika Mkoa wa Singida na Mkoa wa Dodoma na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawa-encourage Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishapu, mahitaji ya mbegu za alizeti za Halmashauri yake wayalete kimaandishi ili sisi tuwapelekee katika ofisi zao za Halmashauri badala ya kufungua ofisi katika eneo hilo linalohusika.