Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 116 2022-02-14

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa utoaji wa mbegu bora za alizeti ili kuongeza uzalishaji wenye tija kwa Wakulima katika Wilaya ya Kishapu?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ni miongoni mwa Halmashauri zenye fursa ya uzalishaji wa zao la alizeti nchini. Kutokana na umuhimu wa nchi kujitosheleza kwa mafuta ya kula, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi inatekeleza Kampeni ya Kitaifa yenye lengo la kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti kwa kuimarisha utafiti, kuongeza uzalishaji wa mbegu bora, kutoa elimu bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeongeza bajeti ya Taasisi yetu ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kutoka Shilingi bilioni 7.5 kwa mwaka 2020/2021 hadi kufikia Shilingi bilioni 11.6 kwa mwaka 2021/2022 na bajeti ya Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) kutoka Shilingi bilioni 5.42 kutoka 2020/2021 hadi kufikia Shilingi bilioni 10.8 kwa ajili ya utafiti na uzalishaji wa mbegu bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mikakati hiyo upatikanaji wa mbegu bora za alizeti umeongezeka kutoka tani 587 mwaka 2021 hadi tani 2,124 mwezi Januari, 2022. Kati ya hizo ASA imesambaza tani 1,600 kwa bei ya ruzuku ya Shilingi 3,500 kwa kilo, ambapo tani 48 za mbegu bora za alizeti zimesambazwa katika Mkoa wa Shinyanga na usambazaji wa mbegu unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini kulingana na mahitaji. Aidha, katika msimu wa 2022/2023 Serikali inalenga kuzalisha na kusambaza tani 5,000 za mbegu bora za alizeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Bunge lako tukufu, naomba kutoa wito kwa viongozi katika Mikoa na Halmashauri kuhakikisha kuwa mbegu zinazosambazwa kwa wakulima zinatumika kulingana na malengo yaliyokusudiwa.