Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini serikali itajenga madaraja ya Gunyoda na Baray ikizingatiwa kuwa madaraja haya ni muhimu sana katika kuunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Karatu?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitangulize masikitiko makubwa ya majibu ya Serikali. Mheshimiwa Naibu Waziri aliyejibu swali hili alijibu swali hili hili katika Bunge lililopita. Leo nilipoona swali hili limerudishwa kwa makosa kutoka swali lile la kwanza nililopenda kuuliza nikaacha kwa sababu nimetumiwa jana jioni. Lakini majibu yaliyotolewa ni tofauti kabisa na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri aliyoyatoa kule mwanzo kwenye Bunge lililopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi niiombe tu Serikali kwamba, tunachouliza hapa ni ujenzi wa Daraja la Bunyoda ambalo Serikali imepigiwa kelele kwa miaka tisa. Na Mheshimiwa Naibu Waziri alitoa majibu mazuri sana kwenye Bunge lililopita, kwamba usanifu wa daraja hili ni bilioni moja na milioni mia mbili. Leo jibu lililokuja ni kwenda kufanya usanifu upya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninadhani kama Mheshimiwa Waziri atarejea kwenye majibu yake arejee, lakini kwa Bunge hili linalokuja daraja hili lisipowekwa kwenye bajeti, nadhani nitakuwa naunga mkono bajeti ambayo haina tija kwa wananchi wa Mbulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, ninaomba majibu ya kina ya daraja hili kujengwa kwa sababu Mheshimiwa Naibu Waziri alijibu ndani ya Bunge hili, akisema katika mwaka wa bajeti wa 2022/2023 daraja hili litatengewa fedha bilioni moja na milioni mia mbili ambapo usanifu wake uko tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pil; eneo la Mbulu Mji lina kata 10 vijijini na kata saba mjini. Eneo lote la vijijini lina makorongo makubwa. Ni lini wataalam wa TARURA na TAMISEMI watakwenda katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu ili waweze kujua namna ya kuweza kutatua tatizo la makorongo linalokabili maeneo ya Halmashauri ya Mji wa Mbulu katika maeneo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, baadhi ya maelezo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyatoa tuliyatoa katika Bunge lako Tukufu, na nilishatoa maelekezo katika ngazi za chini. Kwa hiyo kitu ambacho walikuwa wameshatueleza ni kwamba walikuwa bado hawajafanya usanifu, isipokuwa walitupatia zile gharama za awali, kwamba wanakadiri daraja lile litagharimu bilioni moja nukta mbili. Kwa hiyo sisi ambacho tunahitaji ni exactly figure ili tuweze kuliweka katika bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nipokee maoni na maelezo ambayo ameyatoa Mheshimiwa Mbunge, na niahidi kwamba nitalifanyia kazi, kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mama Samia Suluhu haitakuwa tayari kulidanganya Bunge lako Tukufu. Kwa hiyo hilo hatutalipokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu changamoto nyongine za wananchi wa Jimbo la Mbulu kumaliza matatizo ya makorongo kwa kujenga madaraja pamoja na kurekebisha barabara, Mheshimiwa Mbunge na hili tumelipokea, tutaendelea kufanya usanifu pamoja na tathmini na kama ambavyo kiti chako kilieleza siku zilizopita uliopita, tathmini ya awali tumeshaifanya, bado tunakwenda kufanya tathmini ya kina ili kujua ukubwa wa matatizo katika maeneo yote nchini ikiwemo Jimbo la Mbulu, na sisi tutachukua hatua ya kuyakamilisha. Ahsante sana.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini serikali itajenga madaraja ya Gunyoda na Baray ikizingatiwa kuwa madaraja haya ni muhimu sana katika kuunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Karatu?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ili nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo katika Halmashauri au Jimbo la Mbulu halitofautiani na tatizo lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ambapo Daraja la Godegode halipitiki kwa muda mrefu sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba nipate kauli ya Serikali kuhusiana na ujenzi wa daraja hili ambalo limekuwa ni kiungo katika kata za jirani lakini wananchi wamekuwa wakipata shida sana katika kupata usaifiri. Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja ambalo Mheshimiwa Mbunge amelieleza liko katika barabara ambayo inahudumiwa na TANROADS. Lakini kwa kuwa Serikali ni moja na sisi Ofisi ya Rais-TAMISEMI tunafanya kwa ukaribu sana na watu wa TANROADS tumelipokea hilo, na kwa sababu kama ni tathmini ya pamoja tunaifanya wote kwa pamoja, hususan katika zile barabara ambazo zina mwingiliano; kwa hiyo nilipokee na hili, nalo tuahidi tu kwamba tutalifanyia kazi ili kuhakikisha kuwa wananchi wa maeneo hayo wanapatiwa huduma. Ahsante sana.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini serikali itajenga madaraja ya Gunyoda na Baray ikizingatiwa kuwa madaraja haya ni muhimu sana katika kuunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Karatu?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nishukuru sana Serikali kwa kuleta fedha za TARURA zinazojenga Barabara ya kutoka Kambanga kwenda Ifinsi na kutoka Majalila kwenda Ifinsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shukrani zote hizo barabara ile haitakuwa na umuhimu wa aina yoyote kama hakutakuwa na bajeti ya Daraja la Mto Mnyamasi eneo la Ifinsi.

Je, ni lini Serikali itajenga daraja hilo ili iweze kuwasaidia wananchi wa Kijiji cha Bugu ambao hawana mawasiliano kabisa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naye ameomba daraja, na kiukweli madaraja mengi ndiyo hayo ambayo sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI tuliahidi kwamba tunayafanyia tathmini ili kuhakikisha kwamba tunarahisisha usafiri katika maeneo mbalimbali nchini. Na ahadi hiyo tuliitoa ndani ya Bunge kwa sababu maeneo mengi nchi hii yanasumbuliwa zaidi na madaraja, kwa sababu, moja, ya kuharibika, lakini pili, maeneo mengine yana madaraja ambayo wakati wa misimu ya mvua yanakuwa hayafikiki kabisa kwa sababu ni mabovu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo jukumu letu ni kuhakikisha kwamba tunatakiwa tukajenge madaraja ya kudumu ili kuhakikisha kwamba maeneo hayo yanapata huduma hiyo ya usafiri na usafirishaji wa wananchi wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo jambo ambalo amelieleza Mheshimiwa Kakoso lipo katika mipango yetu, na asubiri tu kwamba baada ya mwaka huu wa fedha, naamini yale yako ndani ya bajeti tutayatekeleza. Ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini serikali itajenga madaraja ya Gunyoda na Baray ikizingatiwa kuwa madaraja haya ni muhimu sana katika kuunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Karatu?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa sababu alipofanya ziara jimboni kwangu tuliweza kwenda eneo moja ambako mto umekatika, mawasiliano hayakuwepo na akaahidi kutoa fedha, na bahati nzuri fedha imeshatolewa, lakini mkandarasi aliye pale ni jeuri na hafanyi kazi kama inavyotakiwa, na fedha tayari anayo.

Je, Waziri yuko tayari kutusaidia kumsukuma huyo mkandarasi aifanye hiyo kazi mara moja ili kuepusha shida ya upitaji ya pale kwa sababu sasa hivi mvua zinaendelea kunyesha?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein, Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilifika jimboni kwa Mheshimiwa Hussein na nilishuhudia hayo madaraja mabovu siyo moja tu mengine yameshaanza na kutekelezeka na baadha ya madaraja ambayo nilikuta katika jimbo lake ni madaraja ya miti, ambayo wananchi walikuwa wanalipishwa fedha. Sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tuliagiza fedha hizo ziende, sasa changamoto ambayo imetokea hapa ni mkandarasi kushindwa kufanya kazi kwa wakati. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge moja nimelipokea, lakini pili kutumia Bunge lako Tukufu namuagiza huyu Mkandarasi afanye kazi kwa wakati kinyume na hapo tutavunja mkataba na kupeleka mkandarasi mwingine ili akamalizie hiyo kazi. Ahsante sana. (Makofi)