Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 107 2022-02-14

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je ni lini serikali itajenga madaraja ya Gunyoda na Baray ikizingatiwa kuwa madaraja haya ni muhimu sana katika kuunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Karatu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Korongo la Gunyoda lenye urefu wa mita 70.4 na kina cha mita tano lipo barabara ya Waama-Masieda katika ya kata ya Gunyoda, Halmashauri ya Mji wa Mbulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kutokana na umuhimu wa daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri za Wilaya ya Mbulu, Karatu na Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini imetetenga bajeti katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu ili kufahamu gharama halisi zinazohitajika katika ujenzi wa daraja hilo. Baada ya kukamilika kwa upembuzi na usanifu wa barabara hiyo, Serikali itatafuta fedha kutoka vyanzo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali imekuwa ikifanya matengenezo ya barabara ya Waama – Masieda yenye urefu wa kilomita 19.98 lenye korongo la Gunyoda ambapo katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya kilometa 17.25 za barabara zilifanyiwa matengenezo kwa shilingi milioni 70.25. Kwa upande wa mwaka wa fedha 2021/ 2022 jumla ya kilometa 14.2 zitatengenezwa kwa shilingi milioni 34.22 na Mkandarasi ameanza kazi za matengenezo na zitakamilika mwezi Mei, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya barabara katika Jimbo la Mbulu kulingana na upatikanaji wa fedha, ili kuimarisha upatikanaji wa huduma muhimu za jamii na kiuchumi.