Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga wodi mpya ya akinamama Wilayani Mbozi itakayokuwa na nafasi ya kutosha kwa ajili ya akinamama wengi kujifungua?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Kwa kuwa bado changamoto ni kubwa sana katika hospitali ya Wilaya ya Mbozi, na fedha ambazo tayari zimepelekwa hazijatosha kumaliza changamoto katika wodi ya wazazi. Nilikuwa nataka kufahamu, kwa nini sasa Serikali isifikirie kutuongezea fedha katika mwaka ujao wa fedha ili kuweza kumaliza changamoto zilizopo katika wodi ya wazazi likiwemo suala la upanuzi pamoja na ukarabati?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, wanawake wa Mkoa wa Songwe katika Wilaya za Mbozi, Ileje, Songwe pamoja na Momba tuko vizuri sana katika suala la kuijaza dunia. Kitakwimu, katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi wastani wa watoto 450 huzaliwa kwa mwezi. Kutokana na changamoto hiyo Hospitali hii ya Wilaya ya Mbozi iko katika Kata ya Vwawa, na kata hiyo mpaka sasa hivi ninapoongea hakuna kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, kwa nini sasa Serikali isifikirie kutujengea kituo cha afya katika Kata ya Vwawa ili kupunguza msongamano katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitambue mchango wa Mheshimiwa Mbunge kwa wanawake wa Mkoa wa Songwe; amekuwa akifanya kazi. Ndiyo maana kama unavyoona, katika swali lake la kwanza ambalo ameliuliza hapa, anasema Serikali ifikirie kuongeza fedha kwa ajili ya kusaidia ile wodi ya akina mama na watoto ya Hospitali ya Mbozi ambako yeye mwenyewe safari iliyopita kabla ya Bunge hili alikuwa hapo na ameahidi kulikarabati jengo hilo. Kwa hiyo nimpongeze kwa hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ambacho ninaweza nikakisema ni kwamba Serikali imepokea maoni ya Mheshimiwa Mbunge ambapo katika swali letu la msingi tumejibu kuwa katika mwaka unaofuata tutaweka milioni 50, lakini pia tutazingatia kwa kuangalia vyanzo vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, kuhusu kujenga kituo cha afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Kata ya Vwawa, na hili tumelipokea. Kwa sababu moja ya malengo la Mheshimiwa Rais ni kuhakikisha kwamba tunasogeza huduma kwa wananchi. Kwa hiyo, ombi lake nalo tumelipokea ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia wanawake wa Mkoa wa Songwe na kazi nzuri ambayo wanaifanya ili kuhakikisha tunakisaidia Chama chetu Cha Mapinduzi pamoja na kuwasaidia wananchi ambao wana imani na Serikali yao. Ahsante sana.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga wodi mpya ya akinamama Wilayani Mbozi itakayokuwa na nafasi ya kutosha kwa ajili ya akinamama wengi kujifungua?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa watu wenye ulemavu wanahitaji privacy zaidi na miundombinu rafiki wakati wa kujifungu. Je, Serikali inaonaje ikatenga vyumba maalum ambavyo vitatumika na wanawake hawa wenye ulemavu wakati wa kujifungua pale wanapojitokeza? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa, Mbunge wa Viti Maalum anayewakilisha watu wenye mahitaji maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naye nimpongeze kwa kuwa anafanya kazi nzuri ya kufuatilia watu wenye mahitaji maalum nchi nzima. Hili alilolileta hapa kama swali. Ameeleza vizuri, kwamba watu wenye mahitaji maalum wanahitaji privacy, na je, Serikali tunalionaje hili kama moja ya mahitaji yetu ya msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba tumepokea mawazo na mapendekezo yake, na tutalipeleka katika timu yetu ya wataalam ili kuhakikisha kwamba walau katika baadhi ya hospitali na maeneo yote ambayo huduma ya afya inahitaji tuweze kutenga hivi vyumba maalum ili kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji maalum. Kwa hiyo, tumelipokea na tutalifanyia kazi. Ahsante sana.