Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 106 2022-02-14

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga wodi mpya ya akinamama Wilayani Mbozi itakayokuwa na nafasi ya kutosha kwa ajili ya akinamama wengi kujifungua?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na ujenzi wa Hospitali Mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe itakayogharimu jumla ya shilingi bilioni 12.26 mpaka kukamilika kwake. Hadi kufikia Disemba 2021 shilingi bilioni 9.8 imetolewa, ambapo jengo la OPD limekamilika na ujenzi wa wodi ya mama na mtoto unaendelea na unatarajiwa kukamilika Disemba, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mbozi ambayo kwa sasa inatumika kama Hospitali Teule ya Mkoa wa Songwe.