Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, Serikali imewezesha kwa kiasi gani Maafisa Ushirika kuweza kufanya shughuli zao kwa ufanisi, ikizingatiwa kuwa kumekuwa na msukumo mkubwa sana wa kuanzisha Vyama vya Ushirika?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kazi kubwa katika kusimamia vyama vya ushirika ipo kwenye wilaya zetu. Je, vifaa hivi vilivyozungumziwa vinaelekezwa kwenye Wilaya au Mikoa? (Makofi)

Pili, Taarifa ya Shirika la Ukaguzi (COASCO) ya mwaka 2019/2020 inaonesha ni vyama 6,021 vilifanyiwa ukaguzi, kati ya vyama hivyo ni vyama 289 nivyo vilivyopatiwa hati safi, sawa na asilimia 4.8.

Je, Serikali haioni kwamba ipo haja ya kuwawezesha maafisa ushirika ili waweze kufanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pikipiki hizi 137 zimeelekezwa katika Halmashauri za Wilaya na kama nilivyosema hapo awali, pamoja na hiyo pia Wizara imeona kuna umuhimu wa kuanza kuandaa bajeti ya kutenga fedha za kununua magari kwa ajili ya kusaidia zoezi la ushirika katika mikoa yetu. Kwa hiyo nimuondolee hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii ya ushirika tunaipa thamani kubwa na tunatambua umuhimu wake katika kumuendeleza mkulima wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, la pili ni linalohusu kuiwezesha COASCO kufanya ukaguzi ili kuweza kupata hali halisi ya vyama vyetu vya ushirika hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti yam waka 2021/2022 Serikali tumetenga shilingi milioni 700 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunavifikia vyama vingi vya ushirika na kufanya ukaguzi. Lengo lake ni kuweza kufikia maeneo mengi zaidi kuliko ilivyokuwa awali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Serikali tumeona umuhimu na tumeendelea kuongeza katika eneo hili.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, Serikali imewezesha kwa kiasi gani Maafisa Ushirika kuweza kufanya shughuli zao kwa ufanisi, ikizingatiwa kuwa kumekuwa na msukumo mkubwa sana wa kuanzisha Vyama vya Ushirika?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali imekuwa ikisisitiza uanzishwaji wa vyama vya ushirika, je, Serikali haioni kwamba umefikia wakati kuwahamasisha wananchi wa Mkoa wa Dodoma wakaanzisha ushirika ukizingatia kwamba zao la zabibu ni zao la biashara na ni zao la kimkakati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Dodoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa mazao ambayo Serikali iliyaongeza katika mazao ya kimkakati ni pamoja na zabibu. Serikali inatambua umuhimu wa zao la zabibu katika Mkoa wa Dodoma na manufaa makubwa ambayo wananchi wamekuwa wakiyapata kupitia zabibu. Hivyo, katika kuharakisha maendeleo ya zao la zabibu katika Mkoa wa Dodoma hivi sasa tayari Mrajisi ameanza na zoezi la usajili wa Vyama vya Ushirika vya Msingi 11 na ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wataitisha mkutano wa majadiliano kupitia kamati ambayo imeundwa kwa ajili ya kuja na Chama cha Ushirika ambacho kitasimamia vyama vya msingi, lengo letu ni kuendelea kuipa thamani zabibu ya Dodoma.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tayari mchakato umeanza na muda si mrefu tutakamilisha zoezi hili, na wakulima wa zabibu wa Dodoma watapata nafasi ya kuwa na chombo ambacho kitasimamia zao hili la zabibu katika Mkoa wa Dodoma.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, Serikali imewezesha kwa kiasi gani Maafisa Ushirika kuweza kufanya shughuli zao kwa ufanisi, ikizingatiwa kuwa kumekuwa na msukumo mkubwa sana wa kuanzisha Vyama vya Ushirika?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi nitoe pongezi kwa Wizara ya Kilimo kwa kufuatilia kilimo cha miwa katika Jimbo la Kilombero, na hivi karibuni Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwa kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Serikali kuendelea kuboresha ushirika bado kuna baadhi ya watu wa ushirika ambao wanalalamikiwa na wakulima, hususan katika Jimbo la Kilombero.

Je, Waziri ama Naibu Waziri atakuwa tayari sasa kuja Kilombero ili kufanya mkutano maalum na wakulima wa miwa na kuwasikiliza kuhusu malalamiko yao kuhusiana na ushirika?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Abubakari na Wabunge wote wa ukanda wa Kilombero, Mtibwa pamoja na maeneo yote hayo, nitakuja mwenyewe binafsi, nitakuja kufanya mikutano na wakulima, nitafanya mikutano na viongozi wa Ushirika na makampuni ili tuweze kuyaondoa matatizo yaliyoko kwenye eneo hilo. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, Serikali imewezesha kwa kiasi gani Maafisa Ushirika kuweza kufanya shughuli zao kwa ufanisi, ikizingatiwa kuwa kumekuwa na msukumo mkubwa sana wa kuanzisha Vyama vya Ushirika?

Supplementary Question 4

MHE.BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, Shirika la COASCO ambalo linashughulika na suala la ukaguzi wa Vyama vya Ushirika nchini limeonekana kuwa na upungufu wa staffs ambao kimsingi ndido wanaosimamia masuala haya ya ukaguzi. Sasa je, Serikali inasema nini kuhusiana na suala hili la kuimarisha COASCO ili suala zima la ukaguzi wa Vyama vya Ushirika ikiwemo vyama vya msingi liweze kufanyika ipasavyo?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Butondo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tunakiri kumekuwepo na udhaifu kwenye COASCO. Hatua tuliyoamua kuchukua kama Wizara na mwelekeo wa Serikali kuanzia mwaka kesho COASCO bajeti yake ya kwenda kukagua Vyama vya Msingi na Vyama Vikuu vya Ushirika itabebwa moja kwa moja na Serikali na hawatoishi kwa kupewa fedha na Vyama vya Ushirika ambao wanakwenda kuwakagua.

Lakini la pili, sasa hivi tunafanya capacity analysis ili tuweze kufikia malengo ambayo tunatakiwa kuyafikia.

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba ule utaratibu wa COASCO kwenda kukagua Chama cha Msingi ama Chama Kikuu na kuhudumiwa na chama, utaratibu huo kuanzia mwaka ujao wa fedha unakufa, bajeti yote ya ukaguzi ambayo ni ya wastani wa bilioni nne itabebwa na Wizara, nao watafanya kazi kama ambavyo tunamtengea fedha CAG.