Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwapatia maji wananchi wa Kijiji cha Fundimbanga, Kata ya Matemanga katika Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante nimeridhishwa na majibu mazuri ya Serikali, lakini je, Naibu Waziri yuko tayari kuja Jimboni kwangu ili kuweza kutembelea miradi hiyo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge Zidadu kwa umahiri wake wa ufuatiliaji wa miradi ya maji. Suala la kuja Jimboni manta hofu, nitafika. (Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwapatia maji wananchi wa Kijiji cha Fundimbanga, Kata ya Matemanga katika Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante; kauli ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ni kumtua ndoo mama kichwani, lakini Tukuyu kuna shida sana ya maji, Serikali ilipanga kutoa fedha shilingi bilioni
4.5 kumaliza tatizo la maji Tukuyu mjini. Lakini mpaka sasa wamepeleka shilingi milioni 500 tu sasa akinamama wa Tukuyu hali ni mbaya sana kutafuta maji.

Sasa je, ni lini Serikali itapeleka hizo fedha kiasi cha shilingi bilioni nne ili kumaliza tatizo la maji Tukuyu mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Mbeya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli na hii si mara ya kwanza Mheshimiwa Suma Fyandomo kufuatilia na amekuwa akifuatilia kwa ushirikiano wa karibu kabisa na Mheshimiwa Mwantona na sisi Wizara ya Maji tumekaa jana, tumeshaweka kwenye mpango tunaongeza shilingi milioni 500 nyingine ili kazi ziweze kuendelea na mgao ujao tutaongeza tena shilingi milioni 500 hadi kuweza kukamilisha mradi huu muhimu kwa sababu Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan lengo ni kuona maeneo yote maji yanapatikana bombani na Tukuyu ni moja ya eneo muhimu sana na Mheshimiwa Mbunge tutafanyakazi kwa pamoja, tutaleta maji kuhakikisha wakinamama wa Tukuyu pia tunawatua ndoo kichwani.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwapatia maji wananchi wa Kijiji cha Fundimbanga, Kata ya Matemanga katika Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Katika Jimbo langu la Kwela Serikali ilileta fedha shilingi bilioni 2.9 kwa ajii ya mradi ndani ya kata ya Ikozi, lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika ni kama umetelekezwa. Nataka nijue commitment ya Serikali ni namna gani ambavyo watawahakikishia ndani ya muda mfupi wananchi wa kata ya Ikozi wanapata maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi yote ambayo tayari utekelezaji unasubiriwa ama umeanza Mheshimiwa Waziri ameshaagiza watendaji wetu mikoani wote kuhakikisha hii miradi inakamilika hivyo Mheshimiwa naomba nikutoe hofu kazi zinakuja kufanyika mradi lazima utekelezwe. Mama Samia anasema kumtua ndoo mama kichwani siyo option, ni lazima. (Makofi)