Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 104 2022-02-11

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuwapatia maji wananchi wa Kijiji cha Fundimbanga, Kata ya Matemanga katika Jimbo la Tunduru Kaskazini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Wilaya ya Tunduru ni wastani wa asilimia 69. Katika kuboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Tunduru, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 inaendelea kuboresha huduma ya maji safi na salama kwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Maji Muhuwesi, Semeni, Ndaje- Mbesa kwa awamu ya pili na ukarabati wa Mradi wa Maji Njenga na Misyaje, ukarabati wa Mradi wa Maji Nalasi na Namwinyu, ujenzi wa Mradi wa Maji Masuguru, upanuzi wa Mradi wa Maji Majimaji, Chalinze, Ligoma, Makoteni na Imani, Kazamoyo na Daraja Mbili.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Matemanga ina jumla ya vijiji vinne, ambavyo ni Milonde, Changarawe, Fundimbanga na Matemanga. Katika vijiji vitatu vinapata huduma ya majisafi na salama kupitia mradi mkubwa wa maji wa Matemanga. Vilevile Kijiji cha Fundimbanga kinapata huduma ya maji kupitia visima virefu viwili vya pampu za mkono, ambavyo havitoshelezi mahitaji kwa wananchi wa kijiji hicho.

Katika kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwenye Kijiji cha Fundimbanga, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imekamilisha utafiti wa maji chini ya ardhi na uchimbaji wa kisima utafanyika mwezi Aprili, 2022. Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji utafanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023.