Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Kalebe utaanza na kukamilika kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 1

MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Swali la kwanza; kwa kuwa huko nyuma nimewahi kuuliza swali hili humu ndani la barabara hii na daraja hili na nikapewa majibu yanayofanana hivyo huko nyuma zaidi ya mara mbili.

Je, ni lini nitapewa majibu ambayo yanatia moyo zaidi na matumaini zaidi kuliko hayo majibu niliyopewa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa barabara hii inafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kama alivyosema Mheshimiwa Waziri na kazi hiyo inakaribia kukamilika, na kwa kuwa barabara hii na daraja hili linahudumia kata 18 kati ya kata 29 za Jimbo langu, na kwa kuwa hii pia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano.

Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa na kukamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini kwa kufuatilia sana hii barabara. Ametaka Serikali impe maneno ya matumaini, naomba niseme siyo tu maneno ya matumaini lakini atakubaliana nami kwamba Wakandarasi sasa hivi wapo site wakiwa wanafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba daraja alilolisema litatekelezwa kwanza kabla halafu wata- submit document lianze kujengwa halafu ndiyo upembuzi na usanifu wa kina wa barabara uendelee wakati daraja hili linajengwa.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Rweikiza awe na imani kwamba kwamba Serikali ya Awamu ya Sita ipo kazini na wananchi wawe na matumaini kwamba walichoahidi Marais kinatekelezwa. Ahsante. (Makofi)