Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 96 2022-02-11

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa Daraja la Kalebe utaanza na kukamilika kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Daraja la Kalebe lenye urefu wa mita 32.56 lipo katika barabara ya Kyaka II – Kanazi – Kyetema yenye urefu wa kilometa 60.65. Barabara hii ni ya Mkoa na inahudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa daraja la Kalebe umejumuishwa katika mradi wa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kyaka II – Kanazi – Kyetema ambao unatekelezwa chini ya Mhandisi Mshauri Luptan Consult Ltd. kwa kushirikiana na Mhandisi Consultancy kwa gharama ya shilingi milioni 340.035. Kazi hii imeanza tarehe 31 Disemba, 2021 na unatarajiwa kukamilika tarehe 30 Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Spika, baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo pamoja na barabara hiyo. Ahsante.