Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya ya Geita Mjini na lini sasa ujenzi huo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi hii ulikuwa ni sehemu ya ujenzi wa barabara miaka sita iliyopita, ambapo ilikuwa ni sehemu ya fedha za mkopo ya World Bank na baada ya muda uli-phase out na fedha hizi zikabaki kwenye Mfuko wa Serikali. Sasa swali langu namba moja; kwa kuwa mkopo huu ulikuwa wa pamoja, fedha zilizobaki kwenye utekelezaji wa mradi huu wa awali zilienda wapi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, nashukuru kwa ujio wa mradi wa pili wa World Bank ambao ni TACTIC ambao unatarajia kuanza hivi karibuni. Sasa kilichosababisha stendi isijengwe awamu ya kwanza ni kwa sababu utangazaji wa miradi unakwenda kwa awamu. Wanatangaza barabara moja baada ya nyingine na mradi mwingine baada ya mwingine na matokeo yake mradi una-phase out na fedha zinaisha. Je, kwa nini Wizara isiwashauri wafadhili, miradi hii ikatangazwa kwa pamoja ili iweze kutekelezwa kwa pamoja kuepuka tatizo lililotokea hapo awali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyingeza ya Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Kanyasu kwa kuwasemea kwa dhati kabisa wananchi wa Geita Mjini. Pili, nimhakikishie kwamba mradi wa ujenzi wa stendi ya kisasa, pamoja na kwamba ulisanifiwa na kupangwa kufanyika pamoja miaka sita iliyopita, changamoto iliyojitokeza ilikuwa ni upungufu wa fedha katika kutelekeza mradi wa stendi hiyo. Stendi hiyo ni ya kisasa, ni kubwa na inahitaji fedha nyingi na ndiyo maana kwenye awamu ile ya kwanza haukuweza kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, kwamba kwenye mwaka wa fedha 2022/2023, tayari usanifu umefanyika na uko hatua za mwisho na utatekelezwa kupitia mradi wa TACTIC ambapo tutajenga barabara za lami kilometa 15 pamoja na stendi hii ya kisasa katika Mji wa Geita. Ahsante sana.

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya ya Geita Mjini na lini sasa ujenzi huo utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa hitaji la stendi lililoko Jimbo la Geita Mjini ni sawa kabisa na lile lililoko katika Jimbo la Mwanga; na kwa kuwa mwezi Novemba mwaka jana Mheshimiwa Rais alipotembelea Mkoa wa Kilimanjaro aliwaahidi wananchi wa Mwanga stendi ya kisasa pale Mwanga.

Swali langu je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais kwa wananchi wake wa Mwanga? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Tadayo, Mbunge wa Mwanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ahadi ya Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan tayari tumeshaipokea Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tumeshaifanyia tathmini na tunatafuta fedha wakati wowote ahadi hiyo itatekelezwa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kazi imeanza kwa ajili ya kujenga stendi ya kisasa pale Mwanga. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya ya Geita Mjini na lini sasa ujenzi huo utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii.

Kwa kuwa hitaji hili la stendi katika Mji wa Geita ni sawasawa na kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Biharamulo cha kupata stendi ya kisasa pale, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa katika Mji wa Biharamulo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa miundombinu ya stendi za kisasa, ujenzi wa barabara pamoja na ujenzi wa masoko vyote ni vipaumbele katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Kazi ambayo Serikali tumeelekeza, kwanza halmashauri zifanye tathmini ya uwezo wa mapato yao ya ndani na kuweka kipaumbele cha kuanza ujenzi wa miundombinu hiyo, zikiwemo stendi za kisasa kwa kutumia mapato ya ndani kwa zile halmashauri zenye uwezo wa mapato ya ndani. Zile halmashauri ambazo hazina uwezo wa mapato ya ndani waandae maandiko ya miradi ya kimkakati ya stendi hizo na kuyawasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na Wizara na Mipango ili tufanye tathmini na kutafuta fedha za kuwezesha kujenga stendi za kisasa za kimikakati katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ezra Chiwelesa kwamba, wafanye tathmini Biharamulo waone uwezo wao wa mapato ya ndani, lakini kama hautoshi walete mradi wa kimkakati ili fedha itafutwe kwa ajili ya kujenga stendi ya kisasa pale Biharamulo. Ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya ya Geita Mjini na lini sasa ujenzi huo utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri; kwa kuwa katika eneo la TaCRI pale Mbimba Vwawa lilitengwa kwa ajili ya kujenga stendi kubwa ya Mkoa wa Songwe. Je, ni lini stendi hiyo itaanza kujengwa? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba baada ya stendi ya mkoa kukosekana katika Mkoa wa Songwe ulifanyika mpango wa kuandaa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Stendi ya kisasa ya Mabasi ya Mkoa wa Songwe katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja. Nimhakikishie kwamba lengo la Serikali bado liko vile vile na mipango inafanyika ya tathmini ya mahitaji ya fedha na kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga stendi ile. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango bado upo na taratibu za kutafuta fedha zinaendelea ili tuanze ujenzi. Nakushukuru sana. (Makofi)