Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 82 2022-02-10

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, nini kinakwamisha ujenzi wa stendi mpya ya Geita Mjini na lini sasa ujenzi huo utaanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi kwenye eneo la ukubwa wa hekta
6.9 unaendelea na upo katika hatua ya usanifu ambapo unafanyika pamoja na usanifu wa miradi mingine ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami nzito zenye urefu wa kilometa 15.4.

Mheshimiwa Spika, kazi za ujenzi wa stendi ya kisasa ya mabasi imepangwa kuanza mwaka wa fedha 2022/2023, baada ya kukamilika kwa usanifu. Mradi huu umepangwa kutekelezwa na Serikali kupitia Mkopo wa Benki ya Dunia. Ahsante.