Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chombo Maalum (Agency) kitakachosimamia shughuli zote za kampuni binafsi za ulinzi ili kuongeza wigo wa kiutendaji pamoja na kuwepo kwa sheria itakayosimamia kampuni hizo?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa vile Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo kwa sheria ya makampuni ya ulinzi binafsi, swali langu ni hili; je, sheria gani kwa sasa hivi inayotumika kuwapatia vibali hayo makampuni binafsi ya ulinzi?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa sasa hakuna sheria mahususi kwa ajili ya kazi hiyo, badala yake inatumiwa miongozo inayotolewa na Mkuu wa Polisi Nchini (IGP).

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chombo Maalum (Agency) kitakachosimamia shughuli zote za kampuni binafsi za ulinzi ili kuongeza wigo wa kiutendaji pamoja na kuwepo kwa sheria itakayosimamia kampuni hizo?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa tunayo makampuni mengi ya binafsi katika nchi yetu: -

Je, ni lini Serikali italeta Muswada wa kuwa na Sheria ya Makampuni Binafsi ya ulinzi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI, WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi ni kwamba mashauriano yanaendelea baina ya Serikali zetu mbili; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili turidhiane. Kwa sababu suala hili linagusa Muungano, hatuwezi kulifanya upande mmoja wa Muungano tukasema tumekamilisha.

Mara taratibu hizo zitakapokamilika, then tutapeleka Muswada kwa ajili ya kupitiwa na kuridhiwa na Bunge.

Mheshimiwa Spika, nashukuru. (Makofi)