Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 80 2022-02-09

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. HAJI AMOUR HAJI aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Chombo Maalum (Agency) kitakachosimamia shughuli zote za kampuni binafsi za ulinzi ili kuongeza wigo wa kiutendaji pamoja na kuwepo kwa sheria itakayosimamia kampuni hizo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Amour Haji, Mbunge wa Pangawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali haioni sababu ya kuanzisha chombo maalumu (Agency) cha kusimamia makampuni binafsi ya ulinzi. Jeshi la Polisi linatosha kusimamia shughuli za makampuni hayo kama ilivyo sasa kwa sababu ndiyo taasisi iliyopewa mamlaka kisheria ya kutoa leseni na hati za umiliki wa silaha hapa nchini ambazo pia humilikiwa na makampuni hayo. Utaratibu huo hutoa urahisi wa kufuatilia mwenendo wa makampuni katika utunzaji na matumizi ya silaha hizo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo kwa sheria itakayosimamia makampuni binafsi ya ulinzi. Tayari mapendekezo ya kutungwa kwa sheria hiyo yapo kwenye hatua zaa awali za mawasiliano baina ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Baada ya maridhiano kati ya Serikali zetu mbili kufikiwa, maandalizi ya sheria hiyo yataendelea kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.