Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na pia Wilaya jirani za Mbarali na Iringa Vijjini lakini pia iko kandokando ya barabara kuu, hivyo kukabiliwa na mzigo mzito wa kuhudumia majeruhi wa ajali zinazotokea kwenye barabara hiyo kama ile ya Mafinga:- Je, Serikali iko tayari kuiongezea hospitali hiyo fedha na watumishi mara mbili zaidi ya kiwango inachopata sasa iweze kuwa na uwezo wa kutosha kukabiliana na mzigo wa kazi?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, jana wakati Wizara ya Afya ina wind-up, wameendelea kusisitiza kwamba Serikali itaajiri watumishi wa kada za afya wanaozidi 10,000 lakini katika jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri katika uhaba wa watumishi 95 anasema tutapewa watumishi 18. Haoni umuhimu wa kuongeza idadi hiyo ikafika angalau watumishi 50 kwa sababu tutaajiri watumishi 10,000?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutarajia michango kutoka CHF ni jambo zuri lakini wote tumeona Wabunge hapa katika michango yao mbalimbali wameelezea ambavyo jambo hili linaendelea kuwa gumu kwa sababu ya kipato duni, lakini pia kutokana na ukosefu wa elimu ya uhamasishaji. Sasa kutarajia fedha kutoka CHF ni kama vile tunaota tu ndoto ambayo inaweza isiwe ya kweli. Kwa hali hiyo, kutokana na mazingira ya hospitali hiyo ambayo nimeshayaeleza, hii fedha iliyotengwa shilingi milioni 90, haitoshi hata on call allowance kwa muda wa miezi mitatu, je, Serikali haioni sababu kwa mazingira hayo ambayo nimeelezea kwamba, Hospitali ya Mafinga iko along the highway, ikaongeza kiwango hicho japo hata theluthi moja ya fedha hizo? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba yetu ya jana Mheshimiwa Waziri wangu wa Afya na Waziri wa Utumishi walielezea suala hili la watumishi ambapo taarifa inaonesha watumishi takribani 10,000 wataajiriwa na maombi ya awali ya kibali kutoka Mafinga yalikuwa yanahitaji watumishi 18. Kwa hiyo, katika mgawanyo wa watumishi hawa 10,000 Halmashauri hii ilikuwa na watumishi 18. Hata hivyo kwa sababu mahitaji ni makubwa tutaangalia tutafanya vipi ili kuondoa matatizo ya wananchi katika sekta ya afya. Kwa hiyo, concern kwamba watumishi 18 watakuwa ni wachache hili tutaliangalia, lakini hayo ndiyo maombi ambayo yametoka katika Halmashauri ya Mafinga.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la ukosefu wa uhamasishaji na kwamba hizi fedha ni ndogo, naomba niwaambie ndugu zangu katika maelekezo yetu mbalimbali tulisema sasa hivi jambo muhimu katika sekta ya afya, ukiachia CHF na mifumo mingine, ni ukusanyaji wa mapato. Nimesema tulivyofanya mazoezi ya kukusanya mapato kwa njia ya electronic mapato yamebadilika sana na jana Waziri wa Afya alikuwa akitoa mifano katika Hospitali ya Mbeya badala ya kukusanya shilingi milioni 70 kwa mwezi sasa inakusanya mpaka shilingi milioni 500. Hospitali ya Sekou Toure pale Mwanza badala ya kukusanya shilingi milioni 150,000 mpaka milioni 200,000 kwa mwezi sasa inakusanya shilingi milioni 3.5 kwa siku. Nenda kule Tumbi badala ya kukusanya shilingi milioni 200,000 kwa siku sasa tunakusanya shilingi milioni nne kwa siku, haya ni mabadiliko makubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili ndiyo maana tunatoa msisitizo kwamba Wabunge tuhakikishe, katika hospitali zote mifumo ya electronic iwe imefungwa ili fedha ziweze kukusanywa na ziende katika mgao sahihi wa kununua vifaa tiba na madawa mwisho wa siku mtaona kila kitu kinaenda vizuri. Tusipozingatia haya, hata tukipeleka fedha bado tutakuwa na matatizo. Kwa hiyo, ajenda yetu kubwa ni kwamba, tutumie mifumo sahihi ya electronic kwa ukusanyaji wa mapato kwa ajili ya huduma ya afya.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na pia Wilaya jirani za Mbarali na Iringa Vijjini lakini pia iko kandokando ya barabara kuu, hivyo kukabiliwa na mzigo mzito wa kuhudumia majeruhi wa ajali zinazotokea kwenye barabara hiyo kama ile ya Mafinga:- Je, Serikali iko tayari kuiongezea hospitali hiyo fedha na watumishi mara mbili zaidi ya kiwango inachopata sasa iweze kuwa na uwezo wa kutosha kukabiliana na mzigo wa kazi?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa matatizo yanayoikumba Mafinga yanafanana kabisa na yale yanayoikumba Hospitali ya Mji wa Kondoa kwa maana ya kwamba Kondoa inahudumia Halmashauri tatu za Kondoa Mjini, Kondoa Vijijini pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Chemba. Je, Serikali ina mpango gani na inafikiria nini katika kuongeza rasilimali fedha na rasilimali watu ili kukidhi mahitaji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hospitali ya Kondoa demand yake imekuwa kubwa na kama nilivyosema awali ajenda yetu kubwa ni kuongeza rasilimali watu pale Kondoa. Concern ya kaka yangu Mheshimiwa Nkamia, Mbunge wa Chemba ni kujenga Hospitali ya Wilaya Chemba ili kupunguza population. Juzi juzi tulivyokuwa tunafungua Hospitali yetu ya Mkoa hapa, Mheshimiwa Nkamia alipeleka ombi maalum kwa Mfuko wa Bima ya Afya Taifa kuangalia uwezekano wa kujenga Hospitali ya Chemba ili kupunguza ile population.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika suala la rasilimali watu tutajitahidi kadri iwezekanavyo kwa huu mgao unaokuja tuangalie Hospitali ya Kondoa tunaisukuma vipi. Hali kadhalika katika suala la rasilimali fedha kama nilivyosema ukiachia hii bajeti ambayo tumeitenga ni lazima sasa twende tukasimamie makusanyo ya mapato kwa nguvu zote. Mifumo hii ya kielektroniki ikitumika vizuri katika sekta ya afya mafanikio yake ni makubwa sana na tutaondoa kero nyingi sana za wananchi katika kupata huduma za afya.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na pia Wilaya jirani za Mbarali na Iringa Vijjini lakini pia iko kandokando ya barabara kuu, hivyo kukabiliwa na mzigo mzito wa kuhudumia majeruhi wa ajali zinazotokea kwenye barabara hiyo kama ile ya Mafinga:- Je, Serikali iko tayari kuiongezea hospitali hiyo fedha na watumishi mara mbili zaidi ya kiwango inachopata sasa iweze kuwa na uwezo wa kutosha kukabiliana na mzigo wa kazi?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba niulize swali dogo. Kwa kuwa Mkoa wa Singida tumejenga Hospitali ya Rufaa na mpaka sasa haijaanza kufanya kazi, je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha hospitali ile inaanza kazi kwa kupeleka vifaa tiba?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli na katika ziara yangu hospitali hiyo ni miongoni mwa hospitali nilizozitembelea wakati wa ziara zangu mikoani na siku ile tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge, miongoni mwa majengo makubwa sana yaliyojengwa ni lile pale Singida Mjini. Nilitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa aliyekuwepo kipindi kile na kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha hospitali ile inafanya kazi. Ukiangalia inawezekana ikawa Hospitali ya Kanda kutokana na ukubwa wake kwa sababu kuna center kubwa ya akinamama kujifungulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kusikitisha jana nilipata taarifa kwamba kuna watu wanataka kutoa vile vitanda kurudisha mjini, natoa agizo hakuna kuondoa kitanda au kitu chochote katika hospitali ile. Wiki ijayo nitakwenda Singida nataka niikute Hospitali ya Singida inafanya kazi. Sitaki kusikia hospitali ambayo uwekezaji wake ni mkubwa na wa mfano, watu wanatoa vitanda kupeleka sehemu zingine, tutawashugulikia watu wote wanaotaka kufanya ubadhirifu katika sekta ya afya.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na pia Wilaya jirani za Mbarali na Iringa Vijjini lakini pia iko kandokando ya barabara kuu, hivyo kukabiliwa na mzigo mzito wa kuhudumia majeruhi wa ajali zinazotokea kwenye barabara hiyo kama ile ya Mafinga:- Je, Serikali iko tayari kuiongezea hospitali hiyo fedha na watumishi mara mbili zaidi ya kiwango inachopata sasa iweze kuwa na uwezo wa kutosha kukabiliana na mzigo wa kazi?

Supplementary Question 4

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa watumishi hawa wanaohamishwa katika sekta ya afya wanacheleweshewa mafao yao huko wanakopelekwa. Je, Serikali itahakikishaje wanapata stahiki zao kwa wakati muafaka?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la malipo ya watumishi, nadhani kama tulivyozungumza awali tutaendelea kuyashughulikia malipo haya hasa kulipa madeni ya watumishi, lakini siyo watumishi pekee hata madeni ya wazabuni mbalimbali ambao wanadai Halmashauri zetu, suala hili tutalifanya kwa pamoja. Lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba tunalipa madeni yote ya watoa huduma aidha watumishi au wale wanaotoa huduma za zabuni katika hospitali zetu na center mbalimbali ili isije kufika muda tukawafunga mikono wakashindwa kufanya kazi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kuna jambo tulizungumzia katika maeneo mbalimbali kwamba kuna pesa ambazo zitakuwa zinatumika kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi. Hata hivyo, naomba kusema kwamba kama hakuna ulazima wa kuhamisha watumishi, tusifanye hivyo kwa sababu tutakuwa tunakuza madeni ya watumishi bila sababu ya msingi.