Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa soko la ujirani mwema katika Kijiji cha Mukarazi ikiwemo miundombinu na ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Pamoja katika Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Nichukue nafasi hii kuishukuru Serikali kwa jinsi ambavyo inaendelea kupambana kuwasaidia wananchi ili waweze kujikwamua kiuchumi: -

Mheshimiwa Spika, soko hili la ujirani mwema ni soko kati ya nchi ya Tanzania na Burundi. Kama nilivyouliza kwenye swali langu la msingi, mahali pale Serikali imeweka pesa kujenga yale mabanda kwa ajili ya biashara, lakini hakuna kituo cha polisi, hakuna TRA, wala hakuna uhamiaji, hivyo, kufanya utendaji wa soko lile kuwa hafifu kwa sababu ya hatarishi hii.

Mheshimiwa Spika, kipekee kabisa mpaka uko kilometa tano ndani ya nchi ya Tanzania kwa hiyo, hata pale ambapo uhamiaji wanafanya shughuli zao za kawaida inasababisha usumbufu sana kwa wananchi. Hivyo, napenda kujua ni lini Serikali itaweka vile vipaumbele vya One Stop Centre kama nilivyouliza kwenye swali langu la msingi, ikiwamo forodha? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Florence kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuwasemea wananchi wa Muhambwe, lakini nimhakikishie kwamba, hoja hizi zote ambazo amezileta Serikali imeanza kufanyia kazi, likiwemo suala hili la kupima maeneo ya viwanja 145 kuzunguka soko, ili tuweze kupata maeneo kwa ajili ya kujenga Vituo vya Polisi, Forodha, lakini pia nae neo la Uhamiaji. Kwa hiyo, mara baada ya ramani zile kukamilishwa ambazo tayari mchakato unatarajiwa kuanza wakati wowote, sasa tutaenda kuomba kwenye sekta husika waweze kujenga vituo hivi na kuwezesha soko kufanya kazi vizuri. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa soko la ujirani mwema katika Kijiji cha Mukarazi ikiwemo miundombinu na ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Pamoja katika Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Mji wa Bukoba uko katika mkoa unaopakana na nchi jirani zaidi ya tatu. Je, ni lini Serikali itajenga soko kuu Bukoba Mjini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mji wa Bukoba ni miongoni mwa miji ambayo iko kwenye mpango mkakati ambao utakwenda kujenga masoko, barabara, vituo vya mabasi vya kisasa. Nimpongeze sana Mheshimiwa Oliver Semuguruka, lakini nimpongeze sana Mheshimiwa Stephen Byabato, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, amekuwa mfuatiliaji wa mara kwa mara na Serikali iko kwenye hatua za mwisho za kuanza utekelezaji wa mradi huo. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba, soko hilo, lakini pamoja na maeneo hayo mengine yatafayiwa kazi baada ya mradi huo kuanza. Nakushukuru sana.