Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 68 2022-02-09

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa soko la ujirani mwema katika Kijiji cha Mukarazi ikiwemo miundombinu na ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Pamoja katika Jimbo la Muhambwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Folrence George Samizi, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Soko la Mukarazi ulianza kutekelezwa Juni, 2018 na kukamilika Oktoba, 2020. Ujenzi wa Soko hilo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 442.61 na kwa sasa soko limekamilika kwa asilimia 100 na linatumika mara mbili kwa wiki.

Mheshimiwa Spika, ili kufanya soko hilo kutumika kikamilifu Halmashauri imetoa kiasi cha Shilingi milioni 5.6 kwa ajili ya kupima viwanja 145 katika eneo la soko kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo biashara, huduma za polisi na forodha. Ahsante.