Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi Galapo Tarafa ya Babati ambacho kinajengwa kwa nguvu za Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri yanayotia moyo hasa pale ambapo wananchi wamejitolea kufanya kazi kubwa na Serikali inapounga mkono. Pamoja na majibu hayo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza; kwa kuwa kituo hiki kinahudumia siyo tu Kata ya Galapo, lakini Tarafa nzima ya Babati ikiwemo Kata ya Kashmamire, pamoja na vijiji vya Jirani vya Wilaya za Kondoa na Kiteto: Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kituo hiki kupatiwa gari? Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili: Je, Waziri yupo tayari sasa kuelekeza kwamba kituo hiki kifanye kazi masaa 24 kuliko ilivyo sasa hivi ambapo kinafungwa saa 12.00 jioni? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya nyongeza mawili ya Mheshimiwa Daniel Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaona umuhimu wa kituo hiki kuwa na gari hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo tutaweza kupata gari za kutosha, tutazingatia maombi yake ya kupeleka gari katika kituo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la pili, kwamba hatuoni sasa kuna umuhimu wa kituo hicho kufanya kazi masaa 24; hili nimelichukua. Tutaangalia hali halisi ya kituo kilivyo kama kinaruhusu kuweza kutoa huduma kwa masaa 24, basi tutafanya hivyo. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi Galapo Tarafa ya Babati ambacho kinajengwa kwa nguvu za Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni miongoni mwa wilaya kongwe lakini haina Kituo cha Polisi mpaka leo sambamba na nyumba za watumishi. Nami kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kutokana na shida hiyo, nimetoa shilingi milioni 10 kusaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali kuwasaidia wananchi wale wapate Kituo cha Polisi? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kutoa shilingi milioni 10 kwa kupitia kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kituo. Nimhakikishie kwamba Serikali tutaelekeza Jeshi la Polisi kupitia utaratibu wa Mfuko wa Tuzo na Tozo kama ambavyo nimejibu katika swali msingi la Mheshimiwa Daniel Sillo ili uangalie uwezekano wa kutumia fedha hizo kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Mbunge katika kuhakikisha kwamba ujenzi wa kituo hiki unaendelea. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi Galapo Tarafa ya Babati ambacho kinajengwa kwa nguvu za Wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la uwepo wa vituo vya polisi kwenye wilaya mbalimbali limekuwa ni changamoto. Tarafa ya kwa Mtoro na Farqwa, Wilayani Chemba tuna kituo kimoja ambacho kipo kwa Mtoro. Kituo kile kimejengwa kwa nguvu za wananchi, ni kwa miaka zaidi ya 10 sasa baadhi ya majengo yamebomoka kutokana na Serikali kutokuunga juhudi za wananchi nguvu zao wanazojitolea. Pia kituo hicho hakina gari kwa ajili ya kuwasaidia polisi kwenda kuhakikisha wanawahudumia wananchi. Je, ni lini Serikali itawapatia fedha kituo cha polisi kwa Mtoro, kwa ajili ya kukarabati na kukamilisha majengo yaliyopo kwa sasa na kuwapatia gari kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu. Lilitakiwa liwe swali moja kwa hiyo nitachagua moja katika haya mawili kwa mwongozo wako.

MWENYEKITI: Ndiyo.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na aidha ni suala la gari ama jengo. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kunti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ya swali hili yanafanana na majibu ya maswali mawili ambayo nimeshayajibu. Kwa hiyo, naomba nirudie majibu yale yale ya maswali mawili ambayo nimeyajibu. Kuhusiana na kwanza pongezi kwa wananchi ambao wameshiriki katika kuunga mkono jitihada za Serikali, kuhakikisha vituo vyetu vya polisi vinajengwa ama vilivyokuwa katika hali mbaya vinakuwa katika hali nzuri, pamoja na kuhakikisha kwamba tunaweza kuwasaidia, askari wetu kuweza kuwa na usafiri kwa ajili ya kuwahudumia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme kwamba kwa kuwa kituo hiki kinahitaji ukarabati, kwanza nitafanya jitihada, aidha, mimi au Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwenda kukitembelea, tuone kituo hiki kiko katika hali gani. Tutakapokuwa tumefika hapo na kuona mazingira tutafikiria, sasa ni njia gani ambayo ni muafaka zaidi ya kuweza kukifanyia aidha ukarabati kituo hiki. Pamoja na suala la usafiri kama ambavyo nimejibu katika maswali mengine ya msingi kwa sasa hivi, gari hatuna lakini tutakapokuwa tumepata gari, basi vilevile tutazingatia na kituo hiki. (Makofi)