Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 61 2022-02-08

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi Galapo Tarafa ya Babati ambacho kinajengwa kwa nguvu za Wananchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mara baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa imani yake na nimwahidi kuwa sitamwangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya shukrani hizo, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mhesimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua na kuthamini michango na jitihada zinazofanywa na wananchi, Wabunge na Viongozi wengine katika kuchangia masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao. Kituo cha Polisi cha Galapo kimejengwa kwa nguvu za wananchi na kwa sasa kimeshapauliwa na kazi iliyobaki ni kuweka milango, madirisha, kupiga plasta, kuweka sakafu pamoja na kupaka rangi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inawapongeza sana wananchi wa Galapo pamoja na Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada zao zilizowezesha ujenzi huo. Kwa njia ya kuunga mkono jitihada hizo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itatumia fedha kutoka kwenye Mfuko wa Tuzo na Tozo katika mwaka wa fedha 2022/2023 ili kukamilisha ujenzi huo.