Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA kama ilivyoahidi katika Vijiji vya Kitayawa, Kipera, Lupalama, Itagutwa, Ikungwe na Lyamgungwe?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kasi ya kusambaza umeme kuwafikia wananchi imekuwa ikisuasua kinyume na ahadi tuliyokuwa tukiambiwa kwamba tutawafikia wananchi wote kwa wakati mmoja; na yote hii inasemekana ni ukosefu wa fedha: Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa hasa vitongoji vya Irangi, Unyangwila, Wambi, Ilongimembe na Igawa pamoja na Kata za Magulirwa na Kihanga? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wakazi wote wanapata umeme? Tumeona kwamba wakileta umeme katika Kijiji wanatoa kwa nyumba tatu au nne halafu wanaruka, wanakwenda sehemu nyingine, wanaruka. Sasa ni mkakati upi wa Serikali wa kuhakikisha kwamba nyumba zote ambazo zinahitaji umeme zinapata? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tendega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kusema kwa niaba ya Serikali kwamba miradi yetu ya REA na upelekaji wa umeme vijijini haisuisui; na hizo rumors kwamba hakuna fedha, siyo za kweli. Katika awamu ya tatu mzunguko wa kwanza, miradi 28; jumla ya Lot 28 zilitekelezwa na asilimia kubwa zimekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi hiki ambacho tupo, jumla ya Lot 39 tayari mikataba yake imesainiwa na takribani shilingi trilioni 1,250 zipo tayari kwenye mikataba na Wakandarasi wanaendelea na kazi katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, suala la uhaba wa fedha halipo. Fedha ipo na umeme utafikishwa katika maeneo yote kwa kadri ya muda ulivyopangwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la pili, ni kweli kwamba siyo kila anayehitaji umeme ameupata kwa sasa, lakini kama ambavyo tumekuwa tukisema hapa, Serikali ya Awamu ya Sita itajitahidi sana kuhakikisha kwamba fedha inapatikana; na mbinu nyingine za ubunifu zimekuwa zikitumika kuishauri Serikali. Tulisema juzi kwamba tunatarajia kufika 2025 kwa kadri tulivyojipanga, Serikali itakuwa imefikisha umeme katika vitongoji vyote kwa kutumia takriba shilingi trilioni 7,500 kama tulivyosema kwamba tutakwenda kutafuta sehemu ya kupata hizo fedha kwa ajili ya kupeleka umeme huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie kwa kumshukuru Mheshimiwa Kiswaga kwa sababu maeneo yote ambayo yamesemwa amekuwa akiyafuatilia pamoja na Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali hilo kwa niaba ya wananchi wa Kalenga. Nashukuru. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA kama ilivyoahidi katika Vijiji vya Kitayawa, Kipera, Lupalama, Itagutwa, Ikungwe na Lyamgungwe?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Japokuwa Serikali imekuwa ikiweka jitihada kubwa kwa kuhakikisha kwamba vijiji vya Mkoa wa Kagera vinapata umeme kupitia REA, lakini ukweli ni kwamba hata kabla ya mgao huu Mkoa wetu wa Kagera umekuwa ukikaa gizani siku mbili, tatu mpaka nne kila wiki na hii inatokana na kwamba bado Mkoa wa Kagera haujaungwanishwa kwenye Gridi ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi cha mwaka 2021 hapa Bungeni niliuliza suala hili na Serikali waliahidi kwamba mwaka 2022 Mkoa wa Kagera utaunganishwa kwenye Gridi ya Taifa. Kwa hiyo, napenda kupata kauli ya Serikali: Je, ni lini Mkoa wa Kagera utaunganishwa kwenye Gridi ya Taifa ili tuondokane na adha ya kuwa gizani? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza swali la Mheshimiwa Neema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kagera unazo Wilaya saba na Wilaya mbili tu za Biharamuro na Ngara ndiyo zinapata umeme wa gridi. Wilaya tano zilizobaki zinapata umeme kutoka Gridi ya Taifa la Uganda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jitihada kubwa sana ambazo zinafanywa na Serikali ni kuhakikisha kwamba Mkoa wa Kagera unaunganishwa na Gridi ya Taifa kwa kutoa umeme katika eneo linaitwa Benako kwa kuchota kwenye line inayotoka katika mradi wetu wa Rusumo kwenda Nyakanazi. Tayari eneo la kupitisha kilometa 179 za line kubwa ya Kilovolt 220 zimeshatengenezwa, survey imeshafanyika na umeme ule utaletwa katika kituo chetu cha kupooza umeme cha Kyaka na Mkoa wa Kagera katika muda mfupi wa miaka miwili utakuwa umeunganishwa katika Gridi ya Taifa. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA kama ilivyoahidi katika Vijiji vya Kitayawa, Kipera, Lupalama, Itagutwa, Ikungwe na Lyamgungwe?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Naomba nimwulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Serikali ina dhamira njema sana ya kupeleka umeme vijijini na kwa kuwa Mkandarasi wa Wilaya ya Manyoni ambapo kuna majimbo mawili; Manyoni Mashariki na Manyoni Magharibi ambapo mimi nipo, Mkandarasi wake alichelewa kuanza kazi na toka ameripoti hatuoni kitu kinachoendelea: Je, Serikali iko tayari kumhimiza aanze kazi haraka?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massare kama ifuatavo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inawahimiza sana Wakandarasi wote kukamilisha kazi zao kwa wakati kwa mujibu wa mkataba na tunaamini hakuna atakayechelewa na atakayechelewa hatua madhubuti zitachukuliwa kwa mujibu wa mkataba.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA kama ilivyoahidi katika Vijiji vya Kitayawa, Kipera, Lupalama, Itagutwa, Ikungwe na Lyamgungwe?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Majimbo mengi yaliyopo mjini, mengine yana kata ambazo zipo vijijini na kuonesha kwamba kata hizo zipo kwenye maeneo ya mjini na umeme wake unatakiwa uwe wa TANESCO. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kata zilizoko kwenye majimbo ya mjini lakini ni kata za vijijini zinapata umeme angalau wa REA ili wananchi hawa waweze nao kunufaika na huduma ya umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba majibu ya uhakika. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ni Serikali sikivu sana. Ninao mpango wa upelekaji wa umeme katika maeneo ya mijini yenye sura ya miji, na mradi huo unaitwa peri-urban. Tayari sasa hivi tangazo limeshatangazwa kwa mikoa minane ya Tanzania Bara kuwapata Wakandarasi watakaopeleka umeme katika maeneo hayo ya peri-urban.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami mwenyewe Jimbo langu la Bukoba Mjini lina maeneo ambayo yanaonekana ni ya mjini lakini yapo vijijini. Kwa hiyo, mradi upo na kabla ya mwaka 2022 kwisha kazi hiyo itakuwa imeanza kufanyika ili kufikisha umeme katika maeneo hayo.