Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 60 2022-02-08

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa REA kama ilivyoahidi katika Vijiji vya Kitayawa, Kipera, Lupalama, Itagutwa, Ikungwe na Lyamgungwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya Kipera, Itagutwa, Ikungwe, Lupalama na Lyamgungwe vimepata umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza. Kazi iliyobaki ni kufikisha umeme katika vitongoji vya vijiji hivyo vilivyobaki bila umeme katika miradi ya ujazilizi (densification) kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO imeshapeleka umeme katika Kitongoji cha Kitayawa ambacho kipo katika Kijiji cha Tagamenda Kata ya Luhota, Wilaya ya Iringa. Aidha, TANESCO pamoja na REA wanaendelea kuunganisha umeme kwa wateja wa Kitongoji cha Kitayawa na vitongoji vingine vya Jimbo la Iringa Mjini na Iringa kwa ujumla kadri ya upatikanaji wa fedha. (Makofi)