Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza: - Je, ni lini mgodi wa makaa ya mawe Kiwira utapata Mwekezaji mpya na kulipa mafao ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi huo?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza napenda kukiambia Kiti chako kwamba Serikali mpaka muda huu walikuwa hawajanipa majibu mimi kama Mbunge kabla ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu niliyopewa na Mheshimiwa Waziri, haki ya mfanyakazi anaposimamishwa hasa kwenye mafao ya PSSSF anatakiwa apewe hata kama kuna mchakato mwingine unaendelea. Ni lini Serikali itasimamia wananchi hao na wafanyakazi hao wa Mgodi wa Kiwira waweze kupata mafao yao wakati michakato mingine inaendelea?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; namwuliza Mheshimiwa Waziri, Mgodi wa Kiwira ulikuwa unaisaidia kiuchumi Wilaya kubwa tatu; Wilaya ya Rungwe yenyewe, Wilaya ya Kyela na Wilaya ya Ileje; sasa hawaoni kuchelewa kuendelea ule mradi unarudisha nyuma maslahi na uchumi wa Wana-Rungwe, Wana-Ileje pamoja na Wana-Kyela? Kwa nini wasifanye haraka na mradi huu ukaanza haraka iwekezanavyo? Ahsante.

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mafao ya wafanyakazi; ni kweli hakuna mtu hata mmoja anafurahia kuona wafanyakazi wale wanapata taabu. Ukweli ni kwamba madai yale yalikuwa ya mwaka 2007, yalifanyiwa uhakiki na Serikali; uhakiki ndiyo umekamilika. Madai yale yalikuwa kuanzia shilingi bilioni 46; yaliyohakikiwa na kuthibitishwa ilikuwa ni shilingi bilioni 1.24. Serikali imekamilisha uhakiki wa madai hayo na sasa yako kwenye utaratibu wa kulipwa pamoja na madai mengine.

Mheshimiwa Spika, tumepiga hatua kubwa sana kuuendeleza mradi huu. Nikiri kwamba Waheshimiwa Wabunge wa maeneo yanayozunguka mgodi huo wamekuwa na msukumo mkubwa sana akiwemo Mheshimiwa Mbunge. Kwa sasa mgodi huo tumeshafanya mabadiliko makubwa mno. Sasa hivi Shirika limeshaujenga na tunazalisha pale Kabulo, lakini kwenye underground mining tayari tuna update, ile underground rail na tayari kiberenge cha kusafirisha tumeshakitengeneza, kinafanya kazi. Tutaanza kuzalisha mwezi huu tani 5,000 kila mwezi na kule Kabulo tutakuwa tunazalisha tani 50,000 kwa mwezi. Nadhani wateja wengi wapo, wananunua makaa ya mawe kutoka kwenye mgodi huo.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza: - Je, ni lini mgodi wa makaa ya mawe Kiwira utapata Mwekezaji mpya na kulipa mafao ya waliokuwa wafanyakazi wa mgodi huo?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nimwulize swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri amefanya kazi kubwa sana, lakini ameendelea kutoa hadithi zile zile. Sasa naomba tujue, ni lini mgodi huu utaanza kuzalisha ile mass production? Ahsante. (Makofi)

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge. Bahati njema yeye mwenyewe katika kipindi kilichopita alitupa hati ya mashaka. Sasa hivi nataka nimwambie hati ile aiondoe kwa sababu tayari uzalishaji umeshaanza.

Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa, itakapofika mwezi Machi mwaka huu 2022 uzalishaji wa mass production wa tani 50,000 kwa mwezi utaanza mara moja.

Mheshimiwa Spika, vile vile underground mining kama nilivyokukwa nikijibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda, tayari tumeshaijenga na kiberenge kinapita na uzalishaji unaanza. Ndani ya mwezi huu tunaanza kuzalisha kwenye mradi wa Kiwira tani 5,000.

Mheshimiwa Spika, Block E na yenyewe tumeanza kuanzisha open pit kwa ajili ya kuchimba. Mgodi huu ulisimama kwa muda mrefu toka mwaka 2008. Ni Awamu ya Sita ya mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa ili mgodi huu uanze na wateja wako wengi, tayari wanapita. Hata barabara ile Mheshimiwa Mbunge alikuwa analalamikia tayari tumeshaijenga. Sasa hivi tunakamilisha lile Daraja la Mwalisi watu waanze kupita pale; na wananchi wa maeneo yale wananufaika na uwepo wa mradi huu. Ahsante.