Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiwalipe angalau robo ya madai Mawakala wa mbolea za ruzuku katika Jimbo la Kalenga?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mawakala wengi nchini wamekuwa wakisaidia sana wakulima kwa kuwakopesha mbolea na hivyo kuleta nafuu sana kwenye upatikanaji wa pembejeo kwa wakulima; sasa suala hili limechukua miaka sita. Kwa mfano kwenye Jimbo langu kuna mama mmoja anaitwa Mama Renata Mbilinyi, anadai shilingi milioni 600 na sasa hivi amekaribia kufilisika: -

Je, Serikali haioni haja ya kuharakisha, kwa sababu jambo hili limechukua muda mrefu, ili kuleta nafuu kwa wakulima wetu? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama maelezo yangu ya awali yalivyosema, ni kwamba hatua za uhakiki zipo mwishoni na pindi zikikamilika, Mawakala wote watalipwa. Kilichochelewesha, kulikuwa na documents zilizokuwa zina- miss, baadhi ya Mawakala wengi walishindwa kuziwasilisha na Serikali iliona kuna umuhimu wa kuwapa muda zaidi kuziwasilisha ili iweze kutenda haki na mtu asidhulumiwe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua zipo mwishoni, zikikamilika Mawakala wote watalipwa.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiwalipe angalau robo ya madai Mawakala wa mbolea za ruzuku katika Jimbo la Kalenga?

Supplementary Question 2

MHE. JULIUS KAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Utaratibu wa ruzuku ulitoa nafuu kubwa sana wa bei za mbolea wakati huo. Hivi tunavyozungumza, bei za mbolea bado ziko juu na hii changamoto bado haijatatuliwa: Je, Serikali inasema nini kwa Watanzania kuhusu bei za mbolea ambapo hadi sasa wanashindwa kuzimudu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, bei ya mbolea ipo juu tofauti na bei ambazo wakulima walinunua katika misimu miwili au mitatu iliyopita. Hata hivyo, Serikali imeendelea kuchukua hatua kuhakikisha kwamba tunampunguzia maumivu mkulima.

Mheshimiwa Spika, katika hatua ya awali kabisa ambayo tumeanza nayo ni kwamba, hivi sasa tumeanza mazungumzo Pamoja na zile kampuni za usambazaji wa mbolea kutoka katika source yenyewe badala ya kuwatumia watu wa katikati, Mheshimiwa Waziri alifanya kikao na Makampuni kutoka Saud Arabia, China Pamoja na Urusi. Lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunaipata mbolea moja kwa moja kutoka kwenye source kuja katika nchi yetu ya Tanzania ili tusiwape nafasi katikati hapa watu ambao wamekuwa wakiongeza bei.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika bajeti inayokuja tumejiandaa kutenga fedha kwa ajili ya stabilization fund kuhakikisha kwamba tuna-control bei ya mbolea ili wakulima wasipate taabu.

Mheshimiwa Spika, la mwisho, tumeendelea kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya mbolea. Ninavyozungumza hivi sasa, kiwanda cha ETRACOM pale Nala Dodoma, kinakamilika mwezi Julai. Kikikamilika kiwanda hiki kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 600,000 za mbolea kwa mwaka na hivyo tutakuwa tumeondoa changamoto hii ya bei ya mbolea kwa wakulima wetu. (Makofi)