Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 48 2022-02-07

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isiwalipe angalau robo ya madai Mawakala wa mbolea za ruzuku katika Jimbo la Kalenga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa madai ya mawakala walioshiriki katika utoaji wa rukuzu ya pembejeo za kilimo kwa msimu wa 2014/2015 na 2015/2016 katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Jimbo la Kalenga. Wakati wa utekelezaji wa Mpango wa Ruzuku, uhakiki wa awali uliofanyika na kubaini kuwepo kwa udanganyifu. Kutokana na hali hiyo, Serikali iliamua kuchukua hatua za kufanya uchunguzi na uhakiki wa kina ili kubaini kiasi halisi cha fedha kinachopaswa kulipwa.

Mheshimiwa Spika, ninapenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa, uhakiki wa madai ya mawakala upo katika hatua za mwisho. Mara uhakiki ukiisha, malipo yatafanyika. (Makofi)