Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI Aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kuunganisha Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi hususan Vijana na kuwa na eneo moja la wazi la utoaji huduma?

Supplementary Question 1

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, la kwanza; kwa kuwa, maelekezo haya yalikuwa ni maelekezo ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge hili la 12 ilifanyika tarehe 13 Novemba, 2020 ni mwaka mzima sasa umepita na zaidi. Na kwa kuwa, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amesema wako katika hatua ya mwisho, swali langu; ningependa sasa Serikali itoe commitment ni lini hasa taarifa hii itakuwa tayari na kuletwa hapa Bungeni kwa ajili ya kuanza utekelezaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na haja ya kuunganisha mifuko hii, lakini changamoto kubwa zaidi ya mifuko hii ni ukosefu wa fedha za kutosha kwa mifuko hii kujiendesha. Sasa ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba, mifuko hii inapokuja kuundwa sasa inakabiliana na changamoto hii na inakuwa na fedha za kutosha kwa ajilinya kukidhi uwezeshaji wa wananchi kiuchumi? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Ng’wasi kwa kuwa, ameendelea kuwasemea sana vijana katika maeneo mengi, ili kuwatetea na kuwawezesaha katika maendeleo ya nchi hii. Ni kweli kama anavyosema ni karibu zaidi ya mwaka sasa tangu maelekezo au jukumu hili tupewe kwa ajili ya kuunganisha mifuko hii.

Mheshimiwa Spika, lakini mtakumbuka kwamba, mifuko hii imegawanyika katika maeneo tofauti, ipo mifuko ile ambayo inatoa mikopo moja kwa moja, lakini ipo mifuko ambayo ni ya dhamana, mingine ni ya kutoa ruzuku na mingine ni ya uwezeshaji, lakini zaidi yah apo mifuko mingine ni ya sekta binafsi. Kwa hiyo, Serikali inafanya tathmini ya kutosha kujiridhisha ili tunapokuja kuona mifuko ipi iunganishwe iwe na tija kweli.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwahakikishie Serikali inaliangalia kwa umuhimu sana na tukikamilisha taarifa hiyo, kama nilivyosema tutaileta hapa Bungeni ili tuweze kuendelea kuboresha mifuko hii.

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili la ukosefu wa fedha za kutosha; ni kweli baadhi ya mifuko imekuwa na changamoto ya kuwa na bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuhudumia wahitaji au kuwawezesha wanaokopa.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema na sisi tulikubaliana ndiyo maana tumesema tunataka kuunganisha mifuko hii ili iweze kuwa kwanza na fedha za kutosha ile ambayo inatoa huduma zinazofanana. Lakini pili mkakati wa Serikali ni kuona kuendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kwa mfano ile kwenye halmashauri ambako tunatoa 10% maana yake mapato yakiimarika yakiongezeka maana yake hata ile 10% itakuwa ni fedha za kutosha zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hiyo ni mikakati ya Serikali kuhakikisha fedha pia zitaendelea kutengwa kwenye mifuko mingine ambayo itakuwa imeunganishwa hapo baadaye ili waweze kuwa na bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI Aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kuunganisha Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi hususan Vijana na kuwa na eneo moja la wazi la utoaji huduma?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara. Kwa kuwa mifuko hii imeonekana haina tija ya kutosha kwa sababu zinatolewa fedha taslim, ni kwa nini sasa Serikali isije na mpango mbadala wa kutoa facilities (vitendea kazi) na kuwawezesha vijana badala ya kuwapa fedha taslimu ambazo pia zimekuwa hazirudi kwenye Serikali lakini pia haziwafikii vijana wa kutosha. Ni kwa nini sasa wasilete utaratibu wa kuwapa vitendea kazi ili waweze kufanya kazi na tuone kitu kinafanyika?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Hanje Mbunge kama ifuatavyo. Ni kweli kumekuwa na changamoto nyingi kama ambavyo nimesema kwa maana ya kutokuwa na fedha za kutosha mahitaji ya wananchi ambao wanataka kukopeshwa au kupata fedha kutoka kwenye mifuko hii. Lakini lengo la Serikali ni lile lile kuimarisha na kuwasaidia kwa ukaribu zaidi wananchi katika kuwawezesha.

Mheshimiwa Spika, moja ya mifuko ambayo inatoa mikopo hii ni NEDF kupitia SIDO pia tumekuwa tukiwapa ujuzi lakini na wengine vitendea kazi. Lakini sasa baada ya kuwa na lengo hili la kuona namna gani kuunganisha mifuko hii naamini taarifa hiyo ndiyo itakuja na utafiti rasmi wa namna gani ya kuboresha ikiwemo kama ni kuwasaidia vitendea kazi hasa vijana ambao wanakuwa wanakopa fedha hizo au wengine na kutokutimisha lengo la mikopo hiyo nakushukuru.