Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara muhimu ya Iboni – Bolisa – Gubalisa iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa barabara hii ya Iboni-Bolisa – Bobali inakabiliwa na athari za mazingira inaendelea kubomoka na kuliwa na maji ambayo yanapita katika mito hii ambapo patakwenda kujengwa vivuko na daraja. Je, Serikali haioni sasa umuhimu wa kulinusuru daraja hili japo kwa kuweka fedha za dharura ili isije ikapata gharama kubwa zaidi ya kujenga daraja badala ya vivuko?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, barabara zetu na madaraja haya ambayo yanakabiliwa na athari za kimazingira kama mmomonyoko wa udongo kutokana na maji yote yanafanyiwa tathmini na kuandaliwa mpango kwanza wa kudhibiti madhara haya yatokanayo na athari za kimazingira, lakini pia yanatengewa fedha kwa ajili ya kujenga vivuko au madaraja kuhakikisha barabara hizi zote zinapitika vizuri.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi kwanza tathmini imefanyika ikiwemo ya kudhibiti mmomonyoko ili barabara ijengwe na kupitika wakati wote. Ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara muhimu ya Iboni – Bolisa – Gubalisa iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.

Mheshimiwa Spika, tunajua Serikali ina mkakati wa kujenga barabara na kuunganisha Mikoa lakini barabara nyingi mnazojenga hamzingatii ile mifumo ya maji kwa hiyo unakuta barabara nyingi mvua inaponyesha magari hayapiti. Mfano ni barabara ya kutoka Dodoma kupitia Mtera kwenda Iringa ni barabara muhimu sana lakini hivi ninavyozungumza mvua ikinyesha barabara haipitiki. Najua kuna ukrabati unafanywa, Je, mna mkakati gani wa kuhakikisha barabara zinapitika wakati wote kwa kuweka mifumo ya maji. Ahsante.(Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, katika ujenzi wa barabara zetu moja ya maeneo ambayo sasa tumeweka kipaumbele, kwanza ni kuhakikisha barabara zetu kwenye designing zinaweka kipengele cha kuweka mifereji ya ku-drain maji ili kuepusha maji kukatisha katika barabara zetu na kuziathiri lakini katika maeneo ambayo madaraja au culvat zinajengwa tumeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba madaraja yanakuwa juu ili kuepusha maji kukatisha katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nikiri kwamba kuna baadhi ya maeneo kulikuwa na changamoto hizo na ndiyo maana sasa designing zetu zote zimeboreshwa kuhakikisha haturudi kwenye changamoto hizo na tutaendelea kutekeleza kwa utaratibu huo. Ahsante.