Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2022-02-07

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara muhimu ya Iboni – Bolisa – Gubalisa iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Iboni – Bolisa – Gubalisa iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kondoa yenye urefu wa kilometa 14.7 inaunganisha maeneo muhimu ya kiuchumi na ni barabara mbadala ya kuingia na kutoka mjini kwa wananchi wanaoelekea Kondoa Vijijini pamoja na Wilaya ya Jirani ya Babati.

Mheshimiwa Spika, barabara hii ina mahitaji ya vivuko vitano na daraja moja ambapo tathmini na usanifu umebainisha kuwa ujenzi wake utagharimu jumla ya shilingi bilioni 2.15. Utekelezaji wa kazi hii umepangwa kufanyika katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa kujenga vivuko na kuiwekea changarawe ili kuiwezesha kutoa huduma katika kipindi chote cha mwaka.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa mpango wa kuiwekea lami haujaandalliwa kutokana na ufinyu wa bajeti.