Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati jengo kongwe la Polisi Wete ambalo lipo katika hali mbaya? (b) Je, ni lini Serikali itayatengeneza magari ya polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba ambapo kwa sasa ni gari moja tu linafanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza ni kwamba kutokana na gharama ya fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa jengo hilo ambalo alisema kwamba ni chakavu lakini jengo hilo ni bovu kabisa.

Je, haoni Mheshimiwa Waziri kwamba kuna haja sasa ya kuambatana na mimi kwenda katika jengo hilo kwenda kujionea na kuona uhalisia wa gharama zinazohitajika katika kutengeneza jengo hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti swali langu la (b) ni kwamba kutokana na ongezeko la vitendo vya udhalilishaji na vitendo mbalimbali vya unyanyasaji wa wanawake na watoto katika eneo la Mkoa wa Kaskazini Pemba na magari ambayo yanatumika ni magari matano tu. Haoni kwamba kuna haja sasa ya kuweza kuongeza magari ya dharura kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vitendo hivi vinakomeshwa muda mfupi ujao? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omar, Mbunge wa Jimbo la Wete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya miongoni mwa wajibu wetu mkubwa ni kuhakikisha kwamba tunakwenda kuona kila jengo ikiwa nyumba za makazi, Kituo cha Polisi, mradi wowote ambao unashughulika na masuala ya Jeshi la Polisi ni wajibu wetu kwenda kuukagua. Nimwambie tu Mheshimiwa Omar kwa kushirikiana na wananchi wa Jimbo la Wete tupo tayari kama Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwenda kukagua na kuona na sio Wete tu, lakini maeneo yote ya Unguja na Pemba na Tanzania kwa ujumla. Ni sehemu ya wajibu wetu na tuko tayari kufanya hivyo na mimi niko tayari kuambatana na yeye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kingine je, sasa si tupate hata gari kwa ajili ya doria na vitendo vya uhalifu? Nimuambie tu Mheshimiwa katika bajeti ambayo tumeisoma ya mwaka 2021/2022 tulisema kwamba tuna jumla ya magari zaidi ya 300 ambayo yatakuja kwa ajili ya Jeshi la Polisi. Nimuambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Jimbo la Wete tutaliangalia kwa jicho la huruma sana kuhakikisha kwamba gari hizo zinakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.