Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 39 2022-02-04

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: -

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati jengo kongwe la Polisi Wete ambalo lipo katika hali mbaya?

(b) Je, ni lini Serikali itayatengeneza magari ya polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba ambapo kwa sasa ni gari moja tu linafanya kazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tena kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Ali Omar, Mbunge wa Jimbo la Wete swali lake lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uchakavu wa jengo la Kituo cha Polisi Wete ambalo limejengwa mwaka
1973. Tathmini kwa ajili ya ukarabati ilifanyika mwaka 2021 na kubaini kwamba kiasi cha shilingi 52,760,000 kinahitajika ili kugharamia ubadilishaji paa, mfumo wa umeme, ceiling board pamoja na kupaka rangi. Hivi sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Kaskazini Pemba kuna magari ya polisi 12 na yanayofanya kazi ni magari matano na magari saba ni mabovu. Tayari magari hayo yameshafanyiwa tathmini ya ubovu na kubainika kuwa kiasi cha shilingi 44,254,000 kinahitajika kwa ajili ya ukarabati. Aidha, ukarabati huo utafanyika kulingana na upatikanaji wa fedha. Nakushukuru.