Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wakandarasi wa Tanzania wanapata fursa ya kujenga Mnara wa Mwalimu Nyerere katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika hasa ikizingatiwa kuwa Serikali ya Tanzania ndio inasimamia ujenzi wa mnara huo?

Supplementary Question 1

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

La kwanza, kwa kuwa ujenzi huu maazimio ya kikao hiki yaliuweka kusimamiwa na Serikali ya Tanzania na kwa kuwa ujenzi wa sanamu hii ya Baba yetu wa Taifa yatasaidia kutangaza utamaduni wa Tanzania na mchango mkubwa wa Baba yetu Taifa katika kupigania uhuru wa nchi mbalimbali za Afrika. Ningependa Serikali ituambie ni kwa nini tangu mwaka 2015 yalipopitishwa maazimio haya mpaka sasa ujenzi huu haujaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, kwa kuwa maamuzi haya au maazimio haya ya kikao yalitoa kipaumbele kwa wakandarasi wazawa wa Tanzania kuwa wa kwanza kabisa kupewa tender hizi na kwa kuwa mwaka 2018 tender hizi zilipotangazwa ilionekana hakuna wasanii/ vijana Watanzania wenye vigezo vya kutosha kimataifa kujenga sanamu hii. Basi Serikali ningependa ituambie ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inakuza ujuzi na uwezo wa wasanii wa Tanzania ili pale tender kama hizi zinapojitokeza kimataifa.

MWENYEKITI: Swali.

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo swali hili.

Ningependa Serikali itueleze ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba wasanii wa Tanzania pale ambapo tender hizi za kimataifa zinatangazwa tena wanajengewa uwezo ili nao wapate kushiriki kama Nchi zingine? Ahsante.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kamani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kamani kwanza amependa kufahamu kwa nini delays. Nipende kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba mchakato huu wa kujenga sanamu ya Baba wa Taifa Ethopia Addis, ilikuwa ni wazo zuri sana kwa wakuu wa nchi za SADC kuipa heshima Taifa letu lakini kumpa heshima Baba wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, delays hizi zinatokana na mchakato; kwanza Kamati lazima ziundwe za kitaifa lakini pia kupitia Kamati hizo lazima zikae na familia ya Baba wa Taifa ili kupata prototypes zile ambazo zinahitajika tatu kabla ya ujenzi wa sanamu hii. Lakini pia conditions ambazo SADC imetupa ni kwamba lazima picha ya Baba wa Taifa iwe ni enzi hizo miaka hiyo wakati anapigania uhuru wa Taifa hili.

Kwa hiyo michakato hii, pamoja na conditions mpaka sasa inaendelea vizuri lengo ikiwa ni kuhakikisha sanamu tutakayoijenga pale Ethiopia iwe ni samanu ambayo inaakisi picha halisi ya Baba wa Taifa. Kwa hiyo, michakato hii inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lako la pili la Mheshimiwa Ng’wasi, ni kwa kiasi gani wasanii wetu tunawashirikisha na tunawajengea uwezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeza Mheshimiwa Mbunge pamoja na Wabunge kwamba mlitupitishia bajeti katika Bunge hili ya zaidi ya shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya sanaa na utamaduni. Kupitia mfuko huu Mheshimiwa Mbunge tukuhakikishie tutaendelea kuwajengea uwezo wasanii wetu, lakini kwa kuwa Tanzania tumepewa nafasi ya kusimamia ujenzi huu wa sanamu ya Baba Taifa, meneja wetu huyu aliyeteuliwa pia amepewa nafasi mbili ya kwenda na wasanii wetu Ethiopia waweze kuona kwamba wasanii wetu waweze kujua teknolojia hii. Kwa hiyo, hii ni Wizara yetu tunalifanyia kazi kwa karibu kupitia Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.