Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 36 2022-02-04

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wakandarasi wa Tanzania wanapata fursa ya kujenga Mnara wa Mwalimu Nyerere katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika hasa ikizingatiwa kuwa Serikali ya Tanzania ndio inasimamia ujenzi wa mnara huo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni Na. SADC/NYERERE ST/02 ilipotangazwa kati ya mwezi Mei na Julai, 2021 ilitoa fursa sawa kwa wakandarasi wote kutoka nchi Wanachama wa SADC. Serikali kupitia Baraza la Sanaa la Taifa ilichukua jitihada za kuwatangazia na kuwahamasisha wadau wote nchini kupitia Shirikisho la Sanaa za Ufundi na Idara za Sanaa za Vyuo Vikuu mbalimbali nchini ili wenye vigezo vilivyoainishwa kwenye zabuni waweze kuomba kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu wapo wakandarasi wa Kitanzania walioomba kazi hii sambamba na wenzao kutoka mataifa wanachama wa SADC. Hivi sasa SADC imekamilisha uchambuzi wa nyaraka na muda wowote mshindi atatangazwa baada ya kusaini mkataba.