Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya mawasiliano ya simu katika Jimbo la Tabora Mjini hususan kwenye kata za pembezoni? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka minara ili kuondoa changamoto hii hasa katika kata ya Itetemia ambayo ina changamoto kubwa ya mawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; pamoja na majimu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo amekiri Jimbo la Tabora Mjini lina sura mbili yaani Kata za Mjini na Kata za Vijijini; changamoto ya mawasiliano ni kubwa sana katika kata za mjini na kata za pembezoni. Kata za vijijini zina vijiji zaidi ya 41, asilimia 75 ya vijiji hivyo haina mawasiliano kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kusema kwamba wamepeleka mawasiliano katika Kata za Kabila na maeneo mengine, lakini Kabila ni pale center ndipo ambapo unapata mawasiliano; lakini kwenye Vijiji vya Igosha, Umanda na vijiji vingine havina mawasiliano kabisa.

Je, Mheshimiwa Waziri ni kwa asilimia ngapi ya vijiji vya kata za pembezoni ambazo tayari mmeshapeleka mawasiliano hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata za Mjini ukiwa katika Kata za Malolo, Ng’ambo na Kidongo Chekundu hupati mawasiliano kabisa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Hawa uliza swali tafadhali.

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti nimtajie kata ambazo zina changamoto na mawasiliano ili aweze kujibu vizuri. Katika kata hizi tatu za Kidongo Chekundu, Ng’ambo na malolo hakuna mawasiliano kabisa tunapokuwa katika kutembelea wananchi maeneo hayo.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha pia mawasiliano katika Kata za Mjini ambazo hazina mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum - Tabora kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala la mawasiliano katika Mji wa Tabora na Serikali inakiri kabisa kwamba Mji wa Tabora ulikuwa na changamoto kubwa ya mawasiliano. Lakini mpaka hapo anaposema Mheshimiwa Mbunge ni kweli kabisa kwamba vijiji vingi havikuwa na mawasiliano, lakini mpaka sasa kuna vijiji vingi ambavyo vimeshapata mawasiliano ambapo tunaamini kabisa kwamba katika utekelezaji wa mpango wa mwaka mmoja mmoja na katika utekelezaji wa miaka mitano tunaamini kabisa kwamba tutakuwa tumefikia katika hatua nzuri kabisa ya kutatua changamoto ya mawasiliano katika kata za pembezoni katika Jimbo la Tabora Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile upande wa kata za mjini; kata za mjini changamoto yake ni moja, ni kwamba kulikuwa na minara ambayo tayari ilikuwa imeshaanza kuzidiwa na tayari Serikali imeshatenga takribani shilingi bilioni 7.6 ambapo tunakwenda kufanya upgrade ya minara takribani 380 nchi nzima; na Tabora Mjini ikiwa sehemu mojawapo ya minara ambayo inakwenda kufanyiwa kazi. Lakini pamoja na hivyo kuna minara ambayo ilikuwa inatoa huduma ya 2G maana yake kwamba hapakuwa na uwezekano wa kupata internet lakini katika mpango huu huu Tabora Mjini tumeiweka katika mpango kabambe ambapo na Mheshimiwa Mbunge tutamshirikisha wakati tukifika Tabora kwa ajili ya kutatua hii changamoto ambayo wananchi wa Tabora wamekuwa wakilalamikia kwa siku nyingi. Ahsante.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya mawasiliano ya simu katika Jimbo la Tabora Mjini hususan kwenye kata za pembezoni? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka minara ili kuondoa changamoto hii hasa katika kata ya Itetemia ambayo ina changamoto kubwa ya mawasiliano?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, lakini pia na kwa kutoa fursa nyingi kwa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi ya nyongeza, tunakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitenga fedha kwa ajili ya kujenga minara tisa ya mawasiliano kwenye Jimbo la Ngara. Naomba kuiuliza Serikali ni lini ujenzi huu wa minara tisa utaanza ili kutatua changamoto ya mawasiliano kwenye jimbo la Ngara? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Serikali ilitangaza kujenga minara tisa katika Jimbo la Ngara katika awamu iliyopita iliyokuwa imetangazwa. Lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, mwezi huu anakwenda kusaini mkataba wa ujenzi wa minara 90 ambayo ni pamoja na minara ambayo itakuwa hapo katikati Jimbo la Ngara.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na subira ili Mheshimiwa Waziri akishakamilisha jambo hili tayari utekelezaji utaanza mara moja. Ahsante.