Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 34 2022-02-04

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza: -

(a) Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya mawasiliano ya simu katika Jimbo la Tabora Mjini hususan kwenye kata za pembezoni?

(b) Je, ni lini Serikali itapeleka minara ili kuondoa changamoto hii hasa katika kata ya Itetemia ambayo ina changamoto kubwa ya mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum - Tabora, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ilifanya tathmini katika Jimbo la Tabora Mjini na kubaini kuwa kata 12 za pembezoni zilikuwa zinahitaji wa kufanyiwa maboresho ya huduma za mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imefikisha huduma za mawasiliano ya simu katika kata tatu za pembezoni ambazo ni Kabila -mtoa huduma ni Halotel; Kalunde na Uyui - mtoa huduma ni Vodacom ndio wamefikisha huduma ya mawasiliano katika maeneo hayo yenye teknolojia ya 2G pekee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ipo katika maandalizi ya awali ya kutangaza zabuni ya kuboresha miundombinu ya minara iliyopo ili iweze kutoa huduma za mawasiliano zenye kutumia teknolojia ya 2G/3G na 4G. Aidha, ujenzi wa minara katika teknolojia ya 2G/3G na 4G unaendelea katika kata tatu za Ndevela, Tumbi pamoja na Itetemia kupitia mtoa huduma Halotel.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna changamoto ya mawasiliano katika Kata ya Itetemia; Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote iliitangaza kata ya Itetemia katika zabuni ya awamu ya nne na kupata mtoa huduma ambae ni Kampuni ya Simu ya Halotel kwa ajili ya kifikisha huduma za mawasiliano ya simu katika kata hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa mnara huo wa simu upo katika hatua za mwisho na unatarajiwa kuanza kutoa huduma kabla ya mwezi Julai, 2022 na utakuwa na teknolojia ya 2G/3G na 4G.